Rais
Jakaya Kikwete, ameagiza utaratibu wa upandishaji wa vyeo kwa wauguzi,
urekebishwe ili wenye sifa wapate stahili zao huku akikemea tabia ya baadhi ya
viongozi wenye tabia ya kuwanyima wafanyakazi haki zao.
Rais
Kikwete alisema hayo jana jijini hapa, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, yenye kaulimbiu
isemayo ‘Wauguzi ni Nguvu ya Mabadiliko na Rasilimali Muhimu kwa Afya’,
yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Shekhe Amri Abeid.
Alisema
ni vyema mfumo huo ukarekebishwa, ili wauguzi wanaojiendeleza wapande vyema na
kuwashangaa baadhi ya watendaji wenye tabia ya kutowapandisha vyeo watumishi
wao, kwa kuhofia nafasi zao kuchukuliwa na wanaojiendeleza.
Mbali
na vyeo, Rais Kikwete alisema pia Serikali itatoa ufadhili kwa wanafunzi wanaosomea Shahada ya Uuguzi
nchini ili kuongeza nafasi ya kuwa na wataalamu wengi wenye sifa za kuwahudumia
wagonjwa kwa moyo wa huruma.
Alionya
kuhusu tabia ya baadhi ya wauguzi wenye tabia ya kutoa lugha za dharau na
kejeli kwa wagonjwa na kusisitiza kuwa uuguzi ni wito, hivyo ni vyema wenye
tabia hiyo, wabadilike na kuanza kutumia
lugha za kufariji wagonjwa.
Alisema
Serikali itaendelea kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwenye zahanati,
wilaya, mkoa pamoja na kusambaza vifaa tiba na kuongeza idadi ya watumishi.
Naibu
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Kwebwe
Stephen Kebwe, alisema utafiti wa idadi ya watu duniani unaonesha kuwa
katika afya kwa mwaka 2010/2013, kumekuwa na ongezeko la uelewa wa matumizi ya
njia za uzazi wa mpango kwa asilimia 96
na kwa wanawake na wanaume asilimia 97.
Pia
alisema vifo vya watoto navyo vikipungua kutoka vifo 165 kwa vizazi hai 1,000
kwa mwaka 1990 hadi kufikia 54 kwa vizazi hai 1,000 mwaka 2013.
Rais
wa Chama cha Wauguzi Tanzania, Paulo
Magesa aliiomba Serikali kuwaboreshea posho wauguzi, ikiwemo fedha kwaajili ya
sare za kazi na kuwapa nyumba, ili watumishi hao wawahi kutoa huduma bora kwa
wagonjwa sehemu mbalimbali.
No comments:
Post a Comment