Watu
wawili wakazi wa Kitongoji cha Kawawa, Manispaa ya Dodoma wamekufa baada ya
kukanyagwa na tembo wenye hasira jana.
Taarifa
iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime watu hao
aliwataja kuwa ni Elizabeth Magawa (80) na Geofrey Mwalabule (7) mwanafunzi
anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Mpunguzi.
Akifafanua
tukio hilo Kamanda Misime alisema kwamba majira ya saa 4 asubuhi jana,
tembo wanane, wakubwa wakiwa saba waliingia katika Kijiji cha Mpunguzi
kilichopo kiasi cha kilomita 20 kutoka Dodoma mjini barabara ya kwenda Iringa.
Alisema
walipoingia tembo hao walianza kula mazao yaliyopo shambani mtama na uwele hali
iliyowafanya wanakijiji waitane na kukusanyika kwa lengo la kuwafukuza
tembo hao.
Anasema
wananchi hao bila kutafuta msaada wa watu wa Mali ya Asili waliwapigia kelele
tembo hao na kuwatupia mawe hali iliyowafanya wakasirike na kucharuka.
Katika
hali hiyo tembo hao waliwakanyaga watu wawili katika Kitongoji cha Kawawa na
kuwaua kisha wakatokomea wakimuacha tembo mtoto.
“Tembo
huyo mtoto kwa sasa analindwa na watu wa Mali Asili akifanyiwa utaratibu wa
kurejeshwa kunakohusika,” alisema Kamanda Misime.
Aidha
Kamanda Misime amesema kwamba juhudi za kutambua tembo hao wametoka mbuga gani
zinaendelea.
Amewataka
wananchi wanapoona tembo au makundi yao watoe taarifa Polisi au Mali Asili na
waache kuwapigia kelele au kuwapiga kwa vitu vyovyote kwani wanaweza kucharuka
na kuleta madhara zaidi.
No comments:
Post a Comment