Licha ya
Serikali kutoa Sh bilioni 1.6 ili kulipa wafanyakazi wa Shirika la Reli la
Tanzania na Zambia (Tazara), bado wamesisitiza kuendelea na mgomo kwa madai
kuwa fedha iliyotolewa ni ya miezi miwili na bado wana madai ya mwezi mmoja.
Akizungumza jana
na mwandishi, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu), Kanda ya Dar
es Salaam, Yusuph Mandai alisema wafanyakazi wamekataa kurudi kazini hadi hapo
watakapolipwa fedha yote.
Alisema fedha
inayodaiwa kupatikana ni ya miezi miwili pekee, Februari na Aprili na umebakia
mwezi mmoja ambao fedha yake haijaingizwa katika akaunti hivyo hawawezi kurudi
kazini.
“Fedha
inayodaiwa kutolewa wafanyakazi hawajaiweka mifukoni, lakini pia bado mwezi
mmoja ambao fedha yake hazikuwekwa,” alisema Mandai.
Alisema
wafanyakazi wana nia njema na shirika ila matakwa yao hayajatimizwa kama
inavyostahili na kwa wakati.
Aliitaja fedha
za miezi iliyotolewa kuwa ni ya Februari na Aprili huku ukibaki mmoja na
Serikali ya Zambia inatakiwa kulipa mshahara wa
Machi na Mei.
Mgomo huo
ulianza wiki iliyopita kwa madai ya wafanyakazi hao kulipwa mishahara yao.
No comments:
Post a Comment