Kamati
ya Tanzania kwanza nje ya bunge wanategemea kuanza mkutano mkubwa wa hadhara
kwa Tanzania na Zanzibar utakaoanza Mei
17 hadi 30 mwaka huu.
Hayo
yalisemwa jana na Mwenyekiti wa kamati hiyo Augustino Matefu wakati akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Alisema
lengo la mkutano huo ni kuhamasisha umoja na muungano ulioasisiwa na hayati
Julius Nyerere na Abeid Karume.
Pia
alisema wanatazamia kupinga mwenendo ambao ulioneshwa na bunge la katiba na
limeonesha jinsi gani wajumbe hawana mapenzi ya dhati ya kupatikana kwa katiba
mpya.
“Tumeona
rais wetu (Jakaya Kikwete) alivyokuwa na nia ya dhati kwetu kutupatia katiba
mpya lakini naona wajumbe wameweka maslahi ya vyama vyao mbele na si nchi,”
alisema Matefu.
Aliongeza
kuwa wameshangazwa kuona kuwa baadhi ya wajumbe wameamua na kukubali kutumiwa
na Nchi za Magharibi kwa lengo la kuigawa nchi vipande vipande.
Aidha
alisema wao kama vijana wazalendo wameweka utaifa mbele na vyama baadaye
kulipinga jambo hili kwa hoja na kwa gharama yoyote.
No comments:
Post a Comment