Serikali
imesema mabadiliko ya tabia nchi pamoja na mwingiliano wa safari yamesababisha
kuwepo kwa ugonjwa wa dengue nchini ambapo hatua mbalimbali za kukabiliana nao
zimechukuliwa.
Kufuatia
hali hiyo serikali imewahakikishia wananchi kuwa hakuna atakayekufa kwa ugonjwa
huo kwa kukosa tiba iwapo atakayeona dalili atafika hospitali na kupatiwa
matibabu mara moja.
Kauli
hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Kebwe S Kebwe
wakati akizindua upya kampeni ya Nyota ya Kijani kwa Kanda ya Ziwa
uliofanyika katika uwanja wa Nyamagana.
Katika
kukabiliana na ugonjwa huo, Naibu Waziri huyo ameutaka uongozi wa mkoa
kushirikiana na Sumatra kuhakikisha wanapuliza dawa kwenye vyombo vyote vya
usafiri zikiwemo meli.
Alisema
dawa za upuliziaji zimesambazwa kwenye halmashauri zote katika kukabiliana na
ugonjwa huo ambao hutokana na virusi baada ya ya kuumwa na mbu aina ya aedes
ambao wengi tulizoea kuwa mbu huyo huambukiza homa ya njano.
Alisema
ugonjwa huo uliingia nchini kwa mara ya kwanza mwaka 2010 ambapo watu 40
waliugua lakini idadi hiyo imeongezeka mwaka 2013 kulikuwa na wagonjwa 143 na
hii inaonesha mazalia ya mbu hao yameongezeka.
Alisema
kuna aina tatu za ugonjwa wa dengue ambapo aina ya kwanza alisema ni ile ambayo
huambatana na homa kali na maumivu ya viungo ambapo asilimia 90 ya watu
wamekuwa wakiumwa.
Alisema
aina ya pili ya ugonjwa huo ni ule kutokwa na damu sehemu mbali mbali za mwili
ikiwemo puani, kwenye fizi, mdomoni na kwenye njia ya haja kubwa, na aina
nyingine ni ile ambayo hutokana na shinikizo la damu ambalo hupatikana kwa
kiwango cha chini.
“Ugonjwa
huu mpya kwa Tanzania mlipuko wake umekuja wakati wa mvua za masika hivyo
kuchangia kuongezeka kwa wagonjwa kutokana na mazalia kuongezeka,” alisema na
kuongeza njia pekee ya kukabiliana nao ni kuhimiza usafi wa mazingira.
No comments:
Post a Comment