Mwenyekiti
Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group inayoendesha Shirika la Usafiri Dar es
Salaam (UDA), Robert Kisena ameeleza kushangazwa na upotoshaji uliofanywa na
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika juu ya uhalali wa umiliki wa hisa za shirika
hilo.
Pamoja
na kushangazwa na upotoshaji huo, Kisena amesema Mnyika ni miongoni mwa wajumbe
wa Baraza la Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam walioshiriki katika vikao halali
vilivyojadili hatua zote za kuuza hisa kwa Simon Group.
Mbali
ya upotoshaji huo kulenga kulihujumu Shirika la UDA, Kisena alisema una lengo
pia la kuwahujumu wananchi wa Dar es Salaam, kuhujumu uchumi wa Taifa, lakini
pia umewashitua wadau wanaofanya kazi na Simon Group kuiboresha UDA
zikiwemo taasisi za fedha, wasambazaji wa mabasi na wataalamu kutoka nje.
Kisena
aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu
uendeshaji wa UDA, siku chache baada ya Mnyika kutoa madai mazito bungeni
akiishutumu Serikali kwa kile alichosema imefumbia macho ufisadi aliodai
umefanywa katika uuzwaji wa hisa za UDA kwa Simon Group.
Mnyika
alisema pia anashangazwa na uwepo wa Simon Group kwenye shughuli za uendeshaji
wa UDA na kuitaka Serikali kutaifisha mabasi yote ili kuzuia UDA chini ya Simon
Group kuendelea kutoa huduma za usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.
Kisena
akizungumzia madai hayo ya Mnyika alisema; “Nimeshangazwa sana na maneno haya
ya Mnyika bungeni na nimeridhika kusema kuwa Mbunge huyu anatumiwa na
mfanyabiashara mmoja (jina linahifadhiwa) ambaye tangu 2011 amekuwa akiendesha
mbinu chafu za kuichafua Simon Group.
“Ni
jambo la kusikitisha kuona pamoja na jitihada za kufanya uwekezaji mkubwa wa
zaidi ya Sh bilioni 300 ili kuwaondolea tabu ya usafiri watu wa Dar es Salaam,
Mbunge wa Jimbo la Dar es Salaam anatumika katika kuwahujumu wananchi wake,
jambo linalosikitisha.”
Akizungumzia
madai ya Mnyika kuhusu kuwepo kwa ufisadi UDA, Kisena alisema madai hayo si
mapya kwani yalikuwepo tangu mwaka 2011 hatua iliyosababisha Serikali Kuu
kuagiza wanahisa wa wakati huo, Simon Group, Msajili wa Hazina na Halmashauri
ya Jiji la Dar es Salaam kukutana na kujadiliana.
“Kutokana
na maelekezo hayo ya Waziri Mkuu, tulikutana Novemba 15, 2011 na kujadili
malalamiko yote yakiwemo kwamba Simon Group tumeuziwa UDA kwa bei ndogo. Baada
ya majadiliano ya kina ilikubalika kuwa pamoja na mambo mengine ufanyike upya
uthamini wa bei ya hisa tulizonunua.
“Pamoja
na kuzungumzia hayo tulizungumzia pia namna ya kumaliza migogoro ya UDA,
kurekebisha kasoro zilizokuwa zinajitokeza katika uendeshaji wa shirika ili
kuleta tija na ufanisi si kwa kuliua shirika bali kwa kuliboresha na
kulistawisha zaidi.
“Kwa
kauli moja wanahisa wote tukakubaliana UDA kuendeshwa na Simon Group na
tukakubaliana kuwa na Bodi ya Wakurugenzi ya pamoja ambapo Januari 9, 2012,
Jiji walimteua Mbunge wa Ukonga, Eugene Mwaiposa kuwa mjumbe wa Bodi katika
kikao ambapo Mnyika alishiriki, na wakati huo Serikali iliendelea kufanya
uthamini upya wa bei ya hisa za ununuzi kupitia Kampuni ya KPMG,” alisema.
Kisena
alisema ilipofika Agosti 16, 2013, wanahisa hao wa UDA waliitwa na Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Serikali za Mitaa chini ya Mwenyekiti wake, Dk Hamis
Kigwangalla katika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam na kuzungumzia madai ya
utata juu ya UDA.
“Baada
ya maelezo na ufafanuzi wetu lakini Kamati ya Bunge ilituita Dodoma sisi sote
ili kujadili zaidi suala la uendeshaji wa UDA, lakini walituagiza kuwa kabla ya
kwenda Dodoma kifanyike kikao cha wadau wote muhimu wa UDA chini ya Mkuu wa
Mkoa ili tuweze kuandaa taarifa ya pamoja juu ya mgogoro wa UDA na ufumbuzi
wake.
“Tulifanya
kikao hicho Agosti 28, 2013 tukiwa sisi sote Msajili wa Hazina, Jiji, Kampuni
Hodhi ya Mashirika ya Umma (CHC) na Simon Group, ambapo katika kikao kile, Jiji
walikuja na muhtasari juu ya kikao chao walichokaa Agosti 22, 2013 Mnyika
akiwa mmoja wa wajumbe ambapo walifikia maazimio mbalimbali.
“Miongoni
mwa maazimio yao ni kuamua kuiuzia Simon Group hisa zake 3,631,046 kwa
takribani Sh bilioni 6 ili kufanya shughuli za UDA kusimamiwa kwa ubora
zaidi na wao kupeleka nguvu zao kwenye Mradi wa Mabasi ya Haraka (DART). Hazina
pia walikuja na maazimio ya kuiachia uendeshaji wa UDA Simon Group.
“Baada
ya kikao hicho tuliandika taarifa ya pamoja ya ni mambo yapi tumeyapatia
ufumbuzi na nini hatma ya baadaye ya UDA. Katika majadiliano hayo yote
tulizingatia pia taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG) anazosema Mnyika, na hivyo taarifa hizo za CAG pia si ngeni,” alisema.
Kisena
alisema Agosti 31, 2013 na Septemba 1, 2013, kilifanyika kikao cha pamoja baina
ya wanahisa wa UDA na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Serikali za Mitaa
kikiwashirikisha pia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (Tamisemi), watendaji wakuu wa Jiji la Dar es Salaam, Hazina
na CHC.
“Kutokana
na majadiliano yetu, Kamati iliamua kuwa migogoro yote iishe na migogoro ya bei
ya hisa irekebishwe lakini iliagiza kuwa hayo yote yafanyike huku ikimpa
mamlaka Simon Group kuendelea na uwekezaji kwa kuzingatia sheria ya uanzishwaji
wa UDA. Utekelezaji wa maagizo ya Kamati umefanyika na hakuna tena utata katika
UDA kama Mnyika anavyojaribu kuendelea kutumika kupotosha.”
Kisena
akizungumzia madhara yaliyopatikana na taarifa hizo alisema ni pamoja na wadau
wanaoshirikiana na Simon Group katika kuiboresha UDA zikiwemo taasisi za fedha,
wataalamu na watengenezaji wa mabasi kuingiwa na shaka isiyo na sababu wala
tija.
“Unajua
wadau kama hawa unapoingia makubaliano nao ili kushirikiana katika uendeshaji
wa mradi wenye mtaji mkubwa kama ilivyo sasa kwa UDA ni lazima uwajengee imani
fulani ili waamini kwamba fedha zao au ushirikiano wao ni salama.Waliposikia
habari za Mnyika walituandikia barua kuomba ufafanuzi, jambo ambalo si zuri
sana,” alisema.
Alisema
mbali ya madhara hayo, yapo madhara kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam
wakiwemo wa Jimbo la Ubungo kuingiwa na hofu ya shirika lao wanalolitegemea
sasa kwa usafiri likifika katika maeneo yote ya jiji na kwa saa zote hadi usiku
kufa.
“Huyu
ni Mbunge ambaye hajali maslahi ya wananchi wake, maana anaposema mabasi ya UDA
yakamatwe na yasitoe huduma na Simon Group wafukuzwe maana yake ni kwamba
anashabikia uwekezaji mkubwa wa usafiri kama wa UDA wenye thamani ya Sh bilioni
300 ufe kwa kile anachodai kuwa anatetea Sh bilioni 11 zisipotee.
“Sisi
UDA pamoja na kutoa huduma za usafiri tunachangia pia kwenye huduma nyingine za
jamii kama kuchangia madawati na hata kuwasafirisha wanafunzi kwenda shule
zilizo mbali zikiwemo za Ubungo, ndio maana nasisitiza kuwa kuna mazingira ya
rushwa katika harakati hizi za Mnyika,” alisema Kisena.
Hali
ya uwekezaji ilivyo
Kisena
alisema madai kuwa Serikali imeuza hisa zake zote si sahihi kwa vile hisa za
serikali 3,488,651 sawa na asilimia 23.26 zipo kama zilivyokuwa awali ingawa
sasa zimepanda thamani kutokana na kuongezeka kwa uwekezaji jambo ambalo ni
faida kwa Serikali.
Alisema
kwa upande wa Simon Group sasa ina hisa 11,011,349 baada ya awali kununua hisa
7,888, 303 ambazo ziliongezwa bei baada ya kudaiwa kununuliwa kwa bei ya chini,
lakini baadaye ikanunua tena hisa 3,631,046 zilizokuwa za Halmashauri ya Jiji.
Alisema
mipango ya uwekezaji inaendelea vizuri kukiwa na lengo la kuwezesha UDA kuwa na
mabasi 2,000 hadi mwisho wa mwaka huu na kwamba kwa sasa mabasi 300 yapo
barabarani huku 200 yakiwa kwenye karakana kwa kufanyiwa maandalizi.
“Mabasi
1,500 yataendelea kuingia nchini kwa mabasi 300 kila mwezi na kimsingi haya ni
kama tumeshayalipia maana tumeshafanya oda. Alisema mabasi marefu 50
yataingizwa nchini muda mfupi ujao na yatatoa huduma katika barabara za
Nyerere, Bagamoyo na Kilwa.
No comments:
Post a Comment