Serikali
imesema Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Profesa Alexander Songorwa na
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Matumizi Endelevu ya Wanyamapori, Profesa
Jafari Kideghesho, hawajawahi kufukuzwa kazi ama kuadhibiwa.
Ilisema
hayo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, iliyotolewa na Idara ya Habari
(Maelezo), Dar es Salaam jana.
Taarifa
hiyo ilisema:“Kumekuwa na taarifa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, kwamba
wakurugenzi hao walikuwa wamefukuzwa kazi na Waziri wa Maliasili na Utalii, na
kisha kurejeshwa kwa maelekezo ya Ikulu. Taarifa hizo si sahihi”.
“Hata
hivyo, kutokana na yaliyokwisha kutokea, wanataaluma hawa, Profesa Alexander
Songorwa na Profesa Jafari Kideghesho, kwa hiari yao wenyewe, wamekubali
kuchukua majukumu mengine katika utumishi wa umma kama watakavyopangiwa,”
ilieleza taarifa hiyo ya Maelezo.
Profesa
Songorwa amehamishiwa katika Chuo cha Wanyamapori Mweka mkoani Kilimanjaro kuwa
Naibu Mkuu wa Chuo hicho, wakati Profesa Kideghesho amehamishiwa Hifadhi ya
Taifa ya Selous, ambako atakuwa Meneja Msaidizi wa Mradi.
Taarifa
hiyo ilieleza kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi, kila mtumishi wa umma, anayo
mamlaka yake ya ajira na mamlaka yake ya nidhamu ;na kwamba Mamlaka ya Nidhamu
ya Profesa Songorwa na Profesa Kideghesho, haijawahi kuwachukulia hatua
zozote za kinidhamu. Lakini, baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii kuonyesha
kutoridhika na utendaji wao, Mamlaka yao ya Nidhamu iliwaruhusu kuchukua likizo
zao za mwaka za kawaida. Likizo zao zilipoisha, walirejea kazini kama
kawaida.
No comments:
Post a Comment