Serikali
imetoa tamko juu ya mfululizo wa vitendo vya uchomaji makanisa vilivyoibuka
hivi karibuni na kusema imeagiza dola ikaze uzi kukabili wimbi
hilo.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda alisema juzi bungeni wakati akihitimisha michango ya
wabunge kuhusu bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15 ya ofisi yake iliyopitishwa
jana.
Alisema
kati ya Februari 6 na Mei 5, mwaka huu, jumla ya makanisa matano yamechomwa
moto au kukumbwa na milipuko ya mabomu katika maeneo mbalimbali nchini.
Alitaja
makanisa hayo na maeneo yalikochomwa ni Living Water la Bukoba lililochomwa
Februari 6, Kanisa la Pentekoste la Kihonda Morogoro lililochomwa Machi 3 na
kanisa moja Zanzibar lililokumbwa na mlipuko Februari 19.
Mengine
ni Kanisa la Pentekoste la Mafia lililochomwa Mei 3, Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri la mjini Mwanza lililokumbwa na mlipuko wa bomu Mei 5 mwaka
huu.
“Trend
(mwenendo) hii si nzuri. Nataka niombe radhi wale wote ambao kwa namna moja au
nyingine wanajikuta kwenye purukushani za namna hii,” alisema.
Alisihi
Watanzania kwamba hali hii si nzuri. Alisema nchi hii haikuzoea hali ya
milipuko, lakini imeanza kujitokeza hivi karibuni.
“Tulichofanya
tumeviambia vyombo vya dola vikaze uzi zaidi kidogo kujaribu kuona chanzo ni
nini na tunaikabili namna gani. Vinginevyo vitatupa tabu sana huko
tunakokwenda,” alisema Pinda.
No comments:
Post a Comment