Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda amesema ruksa wabunge kukemea Serikali inapokosea lakini
wasiikatishe tamaa katika mambo mazuri inayoyafanya badala yake waipe
moyo.
Kauli
hiyo aliitoa wiki hii bungeni alipokuwa akihitimisha michango ya wabunge
waliochangia kuhusu bajeti ya mwaka wa fedha wa 2014/15 ya ofisi
yake.
Kauli
hiyo ilikuja kutokana na baadhi ya wabunge hususani wa upinzani, katika
uchangiaji kubeza na kuponda baadhi ya mambo yaliyofanywa na Serikali
ikiwemo barabara zilizojengwa kwa kusema hazina ubora.
“Unafika
mahali unasema, Mungu wangu nifanyeje. Lakini tutaendelea na hizo juhudi.
Tumeshajifunza, wakati mwingine kulaumiwa umiwa ndiyo sehemu ya mambo ilivyo,
tusikate tamaa,” alisema Pinda.
Aliendelea
kusema, “Naendelea kuwaomba wabunge, muendelee kuunga mkono juhudi hizi.
Tukemeeni pale mnapoona tunakosea. Mimi sina ugomvi na hilo. Lakini
msitukatishe tamaa, tutie moyo ili tuweze kufanya vizuri zaidi,” alisema
Pinda.
Pinda
katika ufafanuzi alitoa takwimu mbalimbali kwa wabunge kuonesha juhudi za
Serikali katika kufanikisha maendeleo, hususani kwenye kilimo, nishati,
miundombinu na pato la wananchi na kusema upo uhakika ifikapo mwaka 2025,
Tanzania itakuwa na uchumi wa kati.
Alisema
mwaka 2000 barabara za la lami zilikuwa kilometa 3,900. Uongozi wa awamu ya
tatu ulianzisha miradi 14 yenye kilometa 1,226 na ikamudu
kumaliza miradi saba. Awamu ya nne ilipoingia ilirithi miradi
iliyobaki.
Pia
chini ya awamu ya nne, ilianzishwa miradi mipya 26 sawa na kilometa 1,759
ambazo kati yake, kilometa 1,270.8 sawa na asilimia 72, zimekamilishwa
kwa kiwango cha lami na kubaki kilometa 488 ambazo Serikali inaendelea
nazo.
No comments:
Post a Comment