Wajumbe
wa Bodi ya Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (Rubada), wamehimizwa
kutimiza malengo yote waliyojiwekea katika muda wao wa miaka mitatu kwa
kuongeza ufanisi zaidi wa mamlaka hiyo.
Waziri
wa Kilimo Chakula na Ushirika, Christopher Chiza alitoa changamoto hiyo jijini
Dar es Salaam jana wakati akizindua bodi hiyo. Alitaka wajumbe wake kufikia
malengo waliyojiwekea na kuifanya Rubada kupiga hatua zaidi kimaendeleo.
“Ningependa
kuona mnajiwekea malengo yenu na kutimiza kwa wakati ili mtakapomaliza muda
wenu, mseme mliletea mafanikio mamlaka hii,” alisema Chiza.
Alisema
wizara yake ina imani kubwa na bodi hiyo ambayo Mwenyekiti wake ni
Profesa Lucian Msambichaka, ambaye ni miongoni mwa wachumi waliobobea nchini.
Mbali
ya Profesa Msambichaka, wajumbe wengine katika bodi hiyo ni Profesa Henry
Mahoo, Bashir Mrindoko, Gaspar Luanda, Hosea Mbise, Raphael Dalluti, Dk
Ben Moshi, Eline Sikazwe na Nkuvililwa Simkanga.
Alitaka
bodi hiyo kuharakisha upatakanaji wa sheria mpya ya mamlaka ili shughuli za
uendelezaji Bonde la Rufiji zisikinzane na sheria nyingine.
Uzinduzi
huo pia ulihudhuriwa na Naibu Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Godfrey
Zambi na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Raphael Daluti.
Mwenyekiti
wa Bodi hiyo, Profesa Msambichaka aliahidi kuhakikisha maagizo yaliyotolewa na
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika yanatekelezwa ili kufikia malengo ya
mamlaka.
No comments:
Post a Comment