Baraza
la Taifa na Hifadhi la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), litaendelea kuwachukulia
hatua za kisheria wachafuzi wa mazingira, wakiwemo wanaochimba mchanga katika
maeneo yasiyo rasmi.
Mwanasheria
wa Baraza hilo, Manchare Suguta, alisema hayo jana wakati akizungumza na
waandishi wa habari juu ya utekelezaji wa shughuli za baraza hilo katika
kusimamia mazingira.
Suguta
alisema kuwa baadhi ya maeneo, yamegeuzwa kuwa machimbo ya mchanga wakati
Serikali haijatenga maeneo hayo kwa shughuli hizo za uchimbaji.
"Kwa
mfano yale machimbo yaliyoko maeneo ya Mbezi tumeshawasiliana na OCD wa
Kawe (Mkuu wa Polisi) ili tuanze kuwakamata kwa kuwa wanakiuka
sheria," alisema Suguta.
Alisema
tangu kuanza kwa baraza hilo limechukua hatua mbalimbali za kusimamia sheria
ikiwa ni pamoja na kuzuia uchimbaji holela wa mchanga katika maeneo yasiyo
rasmi ikiwemo mito.
"Mfano
mzuri ni kuyakamata na kuyatoza faini jumla ya malori 76 yaliyokuwa yanachimba
mchanga maeneo mbalimbali yasiyoruhusiwa, lakini pia wamiliki wa malori hayo
walitakiwa kurejesha mazingira ya maeneo hayo katika hali yake ya awali zoezi
ambalo limeshafanyika," alisema.
Hata
hivyo, alisema kuna changamoto kubwa ya uelewa mdogo wa jamii, kuhusu sheria ya
usimamizi wa mazingira, ambapo wamekuwa wakishindwa kutambua kuwa kila mmoja
ana wajibu wa kuishi katika mazingira safi na salama.
Aidha,
alisema kumekuwepo na mkinzano wa sheria za kisekta na ya mazingira, hivyo
kusababisha shughuli katika maeneo ya vyanzo vya maji kufanyika, ambapo
inakinzana na sheria ya mazingira.
Mkurugenzi
wa Idara ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira wa NEMC, Ignance Mchallo,
aliwataka wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa za maendeleo zinazofanyika
katika maeneo yao kupitia mradi wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM).
"Wananchi
wanaweza kuhoji kuhusu vibali mbalimbali ikiwemo cha TAM kupitia uongozi
husika na wawekezaji wanapaswa kuandikisha miradi au shughuli zao
za maendeleo ili zipitie mchakato wa TAM," alisema.
No comments:
Post a Comment