Shirika
la Ndege Tanzania (ATC), lipo karibu kuanza kung’ara hewani baada ya mwekezaji
kutoka Oman, kuwa tayari kuwekeza kwenye shirika hilo na sasa anasubiri
Serikali kukamilisha taratibu zake.
Miongoni
mwa taratibu zinazosubiriwa ni kwa Serikali kulipa madeni makubwa ambayo ATC
ilikuwa inadaiwa, ili kuweka mizania sawa ya vitabu vya hesabu za fedha.
Mwenyekiti
na Rais wa kampuni za Al Hayat Development and Investment LLC za Oman, Sheikh
Salim Bin Abdullah Al Harthy, alisema wana dhamira ya dhati ya kuwekeza hapa
nchini na hasa katika ATC.
“Tunatarajia
kuwekeza kwenye maeneo tofauti katika sekta za mafuta na uendelezaji wa maeneo
ya fukwe, lakini lengo letu kuu ni kuwekeza ATC,” alisema Sheikh Salim na kuwa
awamu ya kwanza watatumia Sh, bilioni 160.
“Mpango
wetu ni kujenga kituo cha mafunzo ya masuala ya ndege, ofisi nzuri kwa ajili ya
ATC, kununua ndege na kufanya shughuli nyingine za maendeleo. Tunatarajia
kufanya haya katika kipindi kifupi kijacho," alisema.
Alifafanua
kuwa kuna wakati Kampuni ya Al Hayat ilikaa kimya kuhusu uwekezaji huo na
ilifanya hivyo ili kutoa nafasi kwa Serikali kukamilisha taratibu zake ikiwemo
kupitia makubaliano yaliyofikiwa kati ya kampuni hiyo na ATC.
Alisema
watendaji wa Kampuni ya Al Hayat wamekuwa wakitembelea Tanzania mara kwa mara,
kufuatilia suala zima katika uwekezaji kwenye ATC.
Shekhe
Salim alisema ni kutokana na hali hiyo, ndiyo maana hata ule mpango wa kununua
ndege aina ya Bombadier, Air Bus na Embraer ulisimama kidogo kwa kuwa mkataba
rasmi wa uwekezaji bado haujafikiwa na kutiwa saini.
Alisema
safari hii wamekuja tena kuitikia mwito wa ATC ili kuendeleza makubaliano
yaliyofikiwa na kuwa taratibu zikikamilika watatia saini mkataba na kuanza
uwekezaji.
No comments:
Post a Comment