Meneja
Biashara ya Mafuta wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura),
Julius Gashaza (pichani kulia) aliyefariki dunia juzi, anatarajiwa kuagwa leo nyumbani kwake
Yombo Vituka, Dar es Salaam.
Shughuli
za kuagwa kwa mwili huo zinatarajiwa kuanza saa 5 asubuhi kabla ya kusafirishwa
kwenda nyumbani kwao wilayani Ngara.
Mmoja
wa wanafamilia ambaye hakutaka jina lake kuandikwa akizungumza kwa majonzi na mwandishi
jana, alisema shughuli za kuagwa mwili huo zitafanyika nyumbani hapo
zikiambatana na misa ya kumuombea.
Awali
ndugu huyo ambaye alikataa kutajwa gazetini, alisema kuwa kifo cha Gashaza ni
pigo kubwa kwa familia hiyo, lakini hawana cha kufanya zaidi ya kuachia Polisi
kufanya kazi yao.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi,
Gashaza aliajiriwa na mamlaka hiyo 2006 akiwa Mkaguzi Mkuu wa Mafuta ya
Petroli.
Mwaka
2013 Gashaza aliteuliwa kuitumikia Mamlaka hiyo katika cheo cha Meneja wa
Biashara kwenye Idara hiyo ya Petroli.
Taarifa
hiyo ilieleza kuwa mnamo Mei 15, mwaka huu Gashaza alisafiri kwenda Dodoma kwa
usafiri wa ndege akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Ewura kwenye kikao cha Kamati
ya Bunge ya Bajeti.
"Baada
ya kikao hicho, alirejea jijini Dar es Salaam Jumamosi Mei 17, 2014 saa
tatu usiku. Asubuhi ya siku iliyofuata, tarehe 18 Mei 2014, uongozi wa Ewura
ulipokea taarifa za kushtua toka kwa familia yake kwamba Gashaza amefariki
dunia," ilieleza taarifa hiyo.
Taarifa
hiyo ilieleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kuratibu taratibu za mazishi, ambapo
utasafirishwa kwenda Wilaya ya Ngara, nyumbani kwao marehemu.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo, alisema Gashaza alikutwa
amejinyonga kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mwangaza Lodge kwa kutumia
tai aliyoiunganisha na waya wa pazia na kuitundika kwenye nondo za dirisha la
chumba namba 113.
Kamanda
Kiondo alisema chanzo cha kifo chake hakijafahamika lakini inasadikiwa kuwa
siku ya Mei 17, aliwaeleza ndugu zake kuwa ana matatizo ya kiofisi ambayo hata
hivyo hakuyaweka wazi.
No comments:
Post a Comment