Mvua
zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini, zimesababisha mfumuko wa bei
wa taifa kwa mwezi Aprili kuongezeka hadi kufikia asilimia 6.3 kutoka asilimia
6.1.
Kwa
mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kuwepo kwa mfumuko huo wa bei
kumetokana na fahirisi ya bei ya bidhaa mbalimbali kuongezeka hadi 150 mwezi
Aprili mwaka huu kutoka 141.59 mwezi Aprili mwaka 2013.
Mkurugenzi
wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa NBS Ephraim Kwesigabo, alisema jana
kuwa mfumuko wa bei wa mwezi Aprili umeongezeka kutokana na baadhi ya
bidhaa za vyakula kuongezeka bei pamoja na bidhaa zisizo za chakula hasa mkaa.
Mchele
unaelezwa kuwa bei yake imepanda kwa asilimia 3.5, mahindi asilimia 2.5, unga
wa muhogo asilimia 4.8, kuku wa kienyeji asilimia 1.3, dagaa asilimia 6.0, samaki
wakavu asilimia 7.8, matunda kwa asilimia 1.4 na karanga asilimia 2.6 .
Mkaa
ambao unaangukia katika kundi la bidhaa zisizo za chakula umechangia kuongezeka
kwa mfumuko wa bei kwa asilimia 4.3, huduma za matibabu asilimia 3.0, dizeli
asilimia 4.4 na gharama ya kusaga nafaka nayo iliongezeka kwa asilimia 6.6.
Kwesigabo
alisema mfumuko wa mwezi Aprili mwaka huu ambao unapimwa kwa kipimo cha mwezi
umeongezeka kwa asilimia 0.7 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 0.6
iliyokuwa mwezi Machi mwaka huu.
Alisema
mfumuko kwa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi umeongezeka hadi asilimia 7.8
mwezi Aprili kutoka asilimia 7.2 ya mwezi Machi mwaka huu.
Alipoulizwa
sababu ya kuongezeka kwa bei hizo, Kwesigabo alisema "Licha ya kuwa
hatujafanya utafiti lakini mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini
zimechangia kuwepo kwa mfumuko wa bei."
Alisema
gharama za usafirishaji wa bidhaa kutoka mashambani kwenda kwenye miji mikuu ya
mikoa imeongezeka hali ambayo imechangia kuwepo kwa ongezeko hilo.
No comments:
Post a Comment