Muswada
wa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari umekamilika baada ya kupitia hatua
zote muhimu na unatarajia kufikishwa bungeni wakati wowote mwaka huu.
Aidha,
Muswada wa Haki ya Kupata Habari, utafiti wake umekamilika na unaandaliwa na wizara
ya katiba na sheria na baada ya maamuzi utafikishwa bungeni kujadiliwa na kuwa
sheria.
Naibu
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia aliliambia bunge
jana wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Ester Bulaya (CCM)
aliyetaka kujua ni lini serikali itapeleka miswada hiyo miwili na kujadiliwa
kisha kuwa sheria.
Alisema
ni kweli mwaka 2007, serikali iliitikia mwito wa wadau mbalimbali wa habari,
waliotaka kuwepo na tofauti za sheria ya huduma ya vyombo vya habari na uhuru
wa kupata habari.
"Serikali
imepokea mapendekezo kutoka kwa wadau, nafurahi kulijulisha bunge lako tukufu
kuwa muswada wa sheria ya kusimamia
vyombo vya habari, umekamilika baada ya kupitia hatua zote muhimu za kuandaa
muswada na taratibu za kuletwa bungeni zinaandaliwa," alisema.
Katika
swali la nyongeza, mbunge wa Nchinga, Saidi Mtanda(CCM) alitaka kujua ni lini
muswada utaletwa bungeni baada ya kuombwa kwa miaka 17 na kusababisha mazingira
ya uhuru wa kupata habari kuwa na changamoto.
Akimjibu,
Nkamia alisema muswada huo utapelekwa wakati wowote kuanzia sasa, kwa
kuzingatia kalenda za bunge la bajeti na wakati wa muswada.
Mtanda
aliungwa mkono na mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR -Mageuzi) na Mbunge
wa Viti Maalumu, Zainabu Vullu (CCM) waliotaka kujua muda maalumu
wa muswada huo kufikishwa bungeni na kuhoji vyombo vya habari
vinapokosea wanashtakiwa kwa sheria gani na hakuna sheria.
Nkamia
alisema akiwa mdau wa habari, atahakikisha kuona waandishi wa habari wanapata
haki zao hivyo utapelekwa bungeni lakini kila jambo lina utaratibu wake.
No comments:
Post a Comment