Mtoto
wa kiume aliyetambuliwa kwa jina la Yunus Abijan (4) amekufa baada ya
kutumbukia katika kisima cha maji kilicho jirani na nyumba yao.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo alisema, tukio hilo ni la juzi saa
8:45 mchana huko maeneo ya Keko Machungwa, Wilaya ya Temeke.
Alisema
mtoto huyo alikutwa akiwa ametumbukia katika kisima hicho ambacho hakikuwa na
mfuniko kinachomilikiwa na Pili Ally.
Mtoto
huyo alikufa wakati akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Polisi Baracks, maiti
amehifadhiwa Hospitali ya Temeke.
Katika
tukio jingine, mwendesha pikipiki aliyetambuliwa kwa jina la Athumani Abdallah
(28), amekufa baada ya kugongwa na lori.
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, ajali hiyo ni ya
juzi saa 5:50 asubuhi katika Makutano ya Barabara ya Tabata na Mandela.
Alisema
gari aina ya Leyland Daf lenye namba T936 BNT lenye tela namba T442 AWM
ikiendeshwa na mtu asiyefahamika akitoka Ubungo kwenda Buguruni
aligongana na pikipiki yenye namba T237 CPM aina ya Sanya iliyokuwa ikiendeshwa
na mtu huyo.
Maiti
amehifadhiwa Hospitali ya Amana na jitihada za kumtafuta dereva wa lori
aliyekimbia baada ya ajali bado zinaendelea. Gari hilo linashikiliwa na polisi
na upelelezi unaendelea.
No comments:
Post a Comment