Mwanafunzi wa darasa la pili, Shule ya Msingi
ya Wailesi mjini Lindi (jina linahifadhiwa) ameunguzwa moto sehemu ya mikono
yake baada ya kufungwa kamba na mama yake mzazi.
Mama wa mtoto huyo, Mwahija Mohamedi (47)
anatuhumiwa kumfunga mikono kwa kamba na kisha kumchoma moto mtoto huyo mwenye
umri wa miaka 8, akimtuhumu kuchukua Sh
2,600.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Lindi, Renatha
Mzinga alitoa taarifa hiyo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ofisini
kwake.
Alisema mwanamke huyo, ambaye ni mkazi wa
mtaa wa Matopeni mjini hapa, alikamatwa
jana na anashikiliwa na polisi na atafikishwa mahakamani leo.
Mwanafunzi huyo kwa sasa yuko katika
Hospitali ya Mkoa ya Sokoine, mjini hapa kwa matibabu.
No comments:
Post a Comment