Migodi 18 ya madini aina ya tanzanite yaliyopo Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara inafutiwa leseni ya uchimbaji baada ya wamiliki wa migodi hiyo kukiuka sheria ya madini.
Migodi inayokumbwa na sakata hilo ni ile iliyopo
katika kitalu B na D na yote iko mpakani mwa kitalu C kinachomilikiwa na
kampuni ya TanzaniteOne.
Akizungumza na mwandishi ofisi kwake, Kamishina
Msaidizi wa madini Kanda ya Kaskazini, Alex Magayane alisema kuwa migodi hiyo
imekiuka sheria iliyowekwa na Wizara ya Nishati na Madini na kupitishwa na
bunge inayowaelekeza wachimbaji kuchimba madini kwa wima na sio vinginevyo.
Magayane alisema kuchimba madini kwa mserereko na
kuingia kuchimba madini katika kitalu C ni ukiukwaji mkubwa wa sheria hivyo ni
lazima sheria ichukue mkondo wake bila ya kuoneana haya.
Kamishina huyo wa madini aliendelea kusema kuwa
mara kwa mara ofisi yake imekuwa ikisisitiza uwajibikaji wa kufuata sheria na
iwapo mmiliki hatafuata sheria ofisi yake haitavumilia hilo.
No comments:
Post a Comment