Mfanyabiashara
Ibrahim Mshana, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,
akikabiliwa na mashitaka ya kusababishia Shirika la Umeme (TANESCO) hasara ya
Sh milioni 1.4.
Mshana
alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka mawili na Mwendesha Mashitaka
Inspekta Jacksoni Chidunda, mbele ya Hakimu Mkazi, Frank Moshi.
Chidunda
alidai kuwa Oktoba 15 mwaka huu Ukonga, Mshana aliingilia huduma zinazotolewa
na Tanesco kwa kuingiza waya kwenye mita namba 24210835377 katika nyumba ya
Azzas Said, mali hiyo ni ya Tanesco ambayo hutumika kwa ajili ya kutoa huduma.
Aliendelea
kudai kuwa, siku hiyo hiyo, Mshana alisababisha hasara ya fedha kwa Tanesco
baada ya kuingiza waya kwenye mita hiyo.
Mshitakiwa
alikana mashitaka na kurudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini. Upande
wa mashitaka ulidai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kesi
itatajwa tena Mei 29 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment