Polisi mkoani Katavi inawashikilia watu watatu wakituhumiwa kumuua kikatili kwa kumchinja dereva wa pikipiki ‘bodaboda’ Frank Joseph (25) mkazi wa Mtaa wa Nsemulwa mjini Mpanda kisha kumpora pikipiki yake.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahri Kidavashari akizungumza kwa njia ya simu jana kutoka mjini Mpanda aliwataja watuhumiwa kuwa ni Charles Kidaha (29), Madia Mtema (40) na Buyenza Jendesha (40) wote wakazi wa Kijiji cha Mwese wilayani Mpanda.
Kidavashari alidai tukio hilo lilitokea Aprili 26, mwaka huu, saa saa 11 jioni kijijini Mpembe katika Tarafa ya Mwese wilayani Mpanda.
Akisimulia Kamanda Kidavashari alidai kuwa siku ya tukio marehemu akiwa na pikipiki aina ya SunLG yenye nambari za usajili T 704 CDQ, alikodiwa na mtu asiyefahamika kwenda mahala kusikojulikana na kesho yake mwili wake ulionekana ukiwa umetelekezwa porini karibu na kijiji cha Mpembe.
Alisema uchunguzi wa Polisi ulibaini kuwa kifo cha dereva huyo kilitokana na kuchinjwa na watu wasiofahamika ambao baada ya kitendo hicho walitoweka na pikipiki hiyo.
Alisema uchunguzi wa Polisi ulibaini kuwa kifo cha dereva huyo kilitokana na kuchinjwa na watu wasiofahamika ambao baada ya kitendo hicho walitoweka na pikipiki hiyo.
No comments:
Post a Comment