Serikali
imepanga kuleta mapendekezo makubwa ya kupunguza misamaha ya kodi katika bajeti
yake inayotarajiwa kusomwa mwezi ujao.
Taarifa
hiyo ilitolewa mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba
wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge Ngara, Deogratias Ntukamazina (CCM).
Katika
swali lake Ntukamazina alitaka kujua mkakati wa Serikali wa kuongeza mapato
yatakayowawezesha kuwaongezea watumishi wake mishahara na pensheni.
Mwigulu
aliwataka wabunge kuyaunga mkono mapendekezo hayo ambayo yatasaidia kuongeza
mapato ya Serikali.
“Serikali
pia ina mpango wa kuleta bungeni sheria itakayowezesha kuwepo kwa utaratibu
bora wa ukusanyaji kodi na kudhibiti ukwepaji wa kodi,” alisema Mwigulu.
Awali
akijibu swali la msingi la Mbunge huyo Mwigulu alisema moja ya
vigezo
vya kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa umma na wastaafu ni ongezeko la mapato
ya Serikali.
“Uzoefu
unaonyesha kwamba kasi ya ongezeko la mahitaji ya jamii na maendeleo ni
kubwa kuliko ongezeko la mapato.
“Kwa
mantiki hii imekuwa ni changamoto ya kuongeza pesheni kwa wastaafu sambamba na
ukuaji wa uchumi.
“Hata
hivyo Serikali itaangalia uwezekano wa kuboresha viwango vya pensheni kwa nia
ya kuhuisha ili wastaafu waweze kupata unafuu wa maisha,” alisema Mwigulu.
Katika
swali lake Ntukamazina aliitaka Serikali iongeze kiwango cha pensheni kwa
wastaafu.
No comments:
Post a Comment