Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali ombi la Mbunge Bahi, Omary
Badwell (CCM), la kusitishwa kuendelea kusikilizwa kwa kesi
ya kuomba na kupokea rushwa ya Sh milioni nane inayomkabili.
Badwel
kwa aliiomba mahakama hiyo kusimamisha usikilizwaji wa shauri hilo, ili
kusubiri uamuzi wa kesi ya kikatiba aliyoifungua Mahakama Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Dar es Salaam.
Akitoa
uamuzi huo jana, Hakimu Mkazi, Hellen Riwa, alisema mahakama haitakuwa na
sababu ya kutoendelea kusikiliza kesi hiyo kwa kuwa hakuna jambo lililoelezwa
na kufanya shauri hilo kusimamishwa.
Alisema
hakuna maelekezo kutoka ngazi ya juu ya kumuelekeza asitishe kesi pia kesi ya
kikatiba, iliyofunguliwa na mshitakiwa kuhoji kifungu cha kisheria haihusiani
na iliyopo mahakamani hapo.
“Uamuzi
wa kesi hiyo inaweza kutolewa wakati kesi hiyo inaendelea au kutumiwa na
watuhumiwa wengine katika siku zijazo hivyo sikubaliani na maelezo ya wakili wa
Badwel, maombi yake yanatupiliwa mbali,” alisema Hakimu Riwa.
Hakimu
Hellen aliahirisha hiyo hadi Juni 12, mwaka huu, mahakama itakapoendelea
kusikiliza mashahidi wa upande wa Jamhuri. Uamuzi , huo ulitolewa wakati
Badwel hakuwepo mahakamani kwa madai yupo mjini Dodoma anahudhuria
vikao vya Bunge.
Kupitia
kwa Wakili wake Mpare Mpoki, Badwell alidai wamefungua kesi hiyo kwa kuwa
kifungu hicho kinapingana na Ibara ya 13(6)(a) ya Katiba, ambayo inampa haki
mtu yeyote kupinga uamuzi wowote ambao anaona utamuathiri.
Aidha
wanaiomba Mahakama Kuu itamke kifungu hicho ni batili na kinapingana na Katiba.
Inadaiwa
kati ya Mei 30 na Juni 2 mwaka 2012, katika maeneo tofauti Dar es Salaam,
mshitakiwa alishawishi apewe rushwa ya Sh milioni nane kutoka kwa aliyekuwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Sipora Liana.
Ilidaiwa, Badwel aliomba rushwa hiyo ili awashawishi
wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), kupitisha
hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani. Pia anadaiwa Juni 2,
2012 katika Hoteli ya Peacock, iliyopo Ilala, alipokea rushwa ya Sh milioni
moja kutoka kwa Sipora.
No comments:
Post a Comment