Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania
(KKKT) Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria, limelaani kulipuka kwa bomu katika
usharika wa Kanisa Kuu Imani, eneo la Nyumba ya Kupumzikia na Kusababisha mtu
mmoja kujeruhiwa.
Kauli ya kulaani kitendo hicho,
imetolewa jana naAskofu wa KKKT Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria, Andrew
Gulle, wakati akizungumza na waandishi wa habari kanisani hapo jana.
Askofu hiyo ametoa mwito kwa Serikali
kuwatafuta watu waliohusika na tukio hilo ili kuwabaini na kuwafikisha katika
vyombo vya sheria.
“Serikali ihakikishe inatokomeza mtandao
huu waugaidi kabla haujaota mizizi na kuondoa amani tuliyoizoea katika nchi
yetu,” alisema Gulle.
Alisema baada ya bomu hilo kulipuka
usiku wa kuamkiajuzi lilimjeruhi mhudumu wa nyumba hiyo ya kupumzikia wageni,
Bernadetha Alfred (25) katika sehemu
mbalimbali za mwili wake miguuni na
usoni ambapo alikimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando na
kufanyiwa upasuaji.
Hata hivyo, Askofu huyo ametoa wito kwa
Wakristo wote kuwa watulivu, wasiogope wala wasitishwe na mashambulizi yanayotendeka.
Alisema tukio la kulipuka kwa bomu
katika eneo lakanisa ni la kwanza kwa mkoa wa Mwanza, lakini yalikwishatokea
katika kanisa la KKKT Mbagala pamoja na kule Arusha lakini hana uhakika kama
lililotokea Mwanza ni mwendelezo wa matukio hayo.
Alisema kwa hivi sasa wanafanya tathmini
ya ulinziwa kanisa na kuyaomba makanisa yao yote kuboresha na kuimarisha ulinzi
wa maeneo yao.
No comments:
Post a Comment