Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, imeiomba Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuirejeshea mara moja halmashauri hiyo Sh milioni 86.8 zilizotumwa kutoka Hazina kupitia Benki Kuu (BoT) baada ya kubainika fedha hizo za mfuko wa barabara hazikuingizwa katika akaunti zake.
Fedha hizo zinatajwa kuwa sehemu ya milioni 210 zilizoingizwa benki katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2011/12, lakini hazikuonekana na ndipo baraza la madiwani lilipounda tume ya madiwani ili kufuatilia fedha hizo kuanzia Agosti 19, mwaka jana.
Waliounda tume hiyo ni Samson Gelewa, Ferdinand Mpogomi, David Matungwa, Albert Kapongo, Mohammed Shaaban na wataalamu wengine wawili katika masuala ya fedha.
Ripoti ya tume hiyo iliyowasilishwa hivi karibuni na Katibu wake, Mpogomi ambaye pia ni diwani wa Kata ya Sekebugoro ilibaini kutokea kwa mapungufu hayo katika fedha za Mfuko wa Barabara. Taarifa ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), imetajwa kuthibitisha mapungufu hayo.
“Hata hivyo kwa mwaka 2011/12 wilaya ya Kishapu katika bajeti yake ya barabara, ilikuwa ni Sh milioni 412 na kulingana na bajeti hiyo vielelezo vilionesha fedha hiyo ilipokewa wilaya ya Kishapu na katika utafiti huo ilithibitika kuwa Shilingi milioni 123.3 ziliingizwa katika mfuko wa barabara wa halmashauri na kiasi cha Shilingi milioni 86.8 hazikuonekana zilipo…tukajiuliza zimekwenda wapi?” alisema Mpogomi.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Wilson Nkhambaku aliwataka madiwani wanapounda kamati, washirikiane na ofisi yake.
Alisema mara nyingi tume wanazoziunda, amekuwa akizisikia bila kufahamu lengo lake. Hata hivyo, alisema anaipongeza tume hiyo kwa kufanya kazi nzuri.
Fedha hizo zinatajwa kuwa sehemu ya milioni 210 zilizoingizwa benki katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2011/12, lakini hazikuonekana na ndipo baraza la madiwani lilipounda tume ya madiwani ili kufuatilia fedha hizo kuanzia Agosti 19, mwaka jana.
Waliounda tume hiyo ni Samson Gelewa, Ferdinand Mpogomi, David Matungwa, Albert Kapongo, Mohammed Shaaban na wataalamu wengine wawili katika masuala ya fedha.
Ripoti ya tume hiyo iliyowasilishwa hivi karibuni na Katibu wake, Mpogomi ambaye pia ni diwani wa Kata ya Sekebugoro ilibaini kutokea kwa mapungufu hayo katika fedha za Mfuko wa Barabara. Taarifa ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), imetajwa kuthibitisha mapungufu hayo.
“Hata hivyo kwa mwaka 2011/12 wilaya ya Kishapu katika bajeti yake ya barabara, ilikuwa ni Sh milioni 412 na kulingana na bajeti hiyo vielelezo vilionesha fedha hiyo ilipokewa wilaya ya Kishapu na katika utafiti huo ilithibitika kuwa Shilingi milioni 123.3 ziliingizwa katika mfuko wa barabara wa halmashauri na kiasi cha Shilingi milioni 86.8 hazikuonekana zilipo…tukajiuliza zimekwenda wapi?” alisema Mpogomi.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Wilson Nkhambaku aliwataka madiwani wanapounda kamati, washirikiane na ofisi yake.
Alisema mara nyingi tume wanazoziunda, amekuwa akizisikia bila kufahamu lengo lake. Hata hivyo, alisema anaipongeza tume hiyo kwa kufanya kazi nzuri.
No comments:
Post a Comment