Serikali
inatarajia kuzindua mpango wa Sh bilioni mia moja unaolenga kufanya ubora wa
elimu kuwa uhai wa madarasa hapa nchini.
Mpango
huo utazinduliwa na Rais Jakaya Kikwete Mei, 10 mwaka huu katika Uwanja wa
Jamhuri mjini hapa.
Hayo
yalisemwa jana na Naibu Mratibu wa Taifa wa Equip Tanzania, James
Ogondiek wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari.
Alisema
lengo kuu la uwekezaji huo ni kuboresha mchakato wa kufundisha na matokeo ya
kujifunza kwa watoto nchini Tanzania.
Alisema
mpango wa kuinua ubora wa elimu Tanzania- Equip Tanzania ni mpango wa
miaka minne unaoongozwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (Tamisemi) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ukiwa na lengo la
kuboresha utoaji wa elimu kwa kuhakikisha watoto wanapata alama bora katika
mitihani yao.
Aidha
kuwawezesha wanafunzi kushiriki kikamilifu kutimiza azma ya kukua na kuchangia
kupata maendeleo ya haraka nchini Tanzania.
Alisema
mpango huo unafadhiliwa na Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la Misaada la
Uingereza (DFID-UKAID) na unafanya kazi katika wilaya 48, shule 3,700 na
utawafikia watoto milioni 2.1.
Alisema
malengo mengine ni kuimarisha uongozi na usimamizi wa shule kuwa na
mwongozo wa kitaifa wa vigezo vya shule bora na kuwaendeleza kitaalamu.
Pia
walimu wakuu na walimu wakuu wasaidizi zaidi ya 7,200 na waratibu elimu kata
755, kuimarisha usimamizi wa elimu katika ngazi za Wilaya na Mikoa ili kusaidia
menejimenti za wilaya na mikoa katika wilaya 48 na mikoa saba kuboresha tija na
ufanisi wa shule na mifumo inayowasaidia katika utoaji wa
elimu.
Alisema
Equip Tanzania inafanya kazi katika mikoa saba ya Tanzania bara ambapo mwaka
2014 shirika hilo ilianza kazi katika mikoa mitano ya Dodoma, Tabora,
Kigoma,Shinyanga na Simiyu na mwaka 2015 watafikia mikoa ya Lindi na Mara.
No comments:
Post a Comment