Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Devotha Kisoka, amesitisha nia yake
ya kutoa uamuzi wa ombi la aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Gabriel
Fuime, anayeomba afutiwe kesi ya mauaji ya watu 27 inayomkabili na wenzake 11
kwa kuwa jalada la kesi hiyo halipo.
Akitoa
uamuzi huo jana, Hakimu Kisoka alisema hawezi kutoa uamuzi wa ombi
hilo kwa kuwa jalada la kesi hiyo lipo Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam
na hajui sababu ya jalada hilo kuitwa huko.
Aliahirisha
kesi hiyo hadi Mei 27 mwaka huu itakapotajwa tena kwa kuwa upelelezi bado
haujakamilika na washitakiwa wataendelea kusota rumande.
Katika
ombi lake alilowasilisha kupitia kwa mawakili wake John Mhozya na Ndurumah
Majembe, Fuime aliiomba Mahakama kuangalia kwa makini hati ya mashitaka kwa kuwa
madai ni batili na hati iliyopo mahakamani haikidhi matakwa ya sheria.
Alidai
kuwa kwa mujibu wa sheria, hati ya mashitaka inatakiwa kuwa na viashiria
vya kosa ambalo mshitakiwa anashitakiwa nalo lakini hati iliyopo
mahakamani haina viashiria vinavyoonesha kosa la mauaji.
Mbali
na Fume washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni mfanyabiashara Laza Radha,
Diwani katika Manispaa ya Kinondoni, Ibrahim Mohamed (59), vigogo wa Manispaa
ya Ilala ambao ni Mhandisi Mkuu, Charles Ogare(48), Mhandisi wa Majengo Godluck
Sylivester (35) na Mkurugenzi Mkuu wa Mkaguzi wa Majengo, Willibrod Mugyabuso
(42).
Wengine
ni Mhandisi Mohamed Abdulkarim (61), Mhandisi Mshauri, Zonazea Oushoshaodaga
Hema (59), Msajili Msaidizi AQRB, Albert Mnuo na Ofisa Mkuu Mtekelezaji OQRB,
Joseph Ringo (60), Mkadiriaji Ujenzi, Vedasto Ruhale (59), Msanifu Majengo,
Michael.
Inadaiwa
kuwa Machi 29 mwaka jana, katika mtaa wa India Gandhi Ilala, Dar es Salaam kwa
makusudi washitakiwa waliwaua watu 27.
No comments:
Post a Comment