Kikosi
dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Kaskazini kimemtia hatiani Ofisa Ushirika wa
Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mji mdogo wa
Mirerani, Nelson Noman Msangi (54) kwa kosa la kukutwa na meno matatu ya tembo
na kipande cha pembe ya faru chenye uzito wa gramu 80 vyote vikiwa na thamani
ya zaidi ya Sh milioni 10.
Mbali
ya Msangi ambaye ni Ofisa wa Serikali mwingine aliyekamatwa naye ni pamoja na
mfanyabiashara maarufu wa jijini Dar es Salaam, Shabani Salumu Mpara
(42).
Meno
hayo ya tembo yalikuwa na thamani ya dola za kimarekani 5,720 sawa na fedha za
kitanzania Sh 9,323,600 na kipande cha pembe ya faru chenye gramu 80 kilikuwa
na thamani ya dola za kimarekani 600 sawa na Sh za kitanzania
978,000 jumla nyara zote zilikuwa na thamani ya Sh 10,301,600.
Wakisomewa
mashtaka na mwendesha mashtaka wa KDU, Michael Msokwa ilidaiwa kuwa watuhumiwa
hao wameshitakiwa kwa makosa mawili ikiwemo kukutwa na nyara za serikali na
kuhujumu uchumi.
Msokwa
aliieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha mbele ya Hakimu Devota Msofe
kuwa watuhumiwa walikutwa na nyara za Serikali mnamo Aprili 4 mwaka huu katika
Kijiji cha Kibilashi Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga kinyume na sheria.
Akizungumza
nje ya Mahakama Msokwa alisema kuwa nyara hizo za washitakiwa zilikamatwa na
gari aina ya Toyota Opa lenye namba za usajili T249BUA baada ya kupata taarifa
kutoka kwa raia wema.
No comments:
Post a Comment