Huduma
katika Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara), zinatarajiwa kurejea leo
baada ya Serikali kupatia ufumbuzi matatizo yaliyosababisha mgomo wa
wafanyakazi kuanzia Jumatatu iliyopita.
Akizungumza
na gazeti hili jana Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaban
Mwinjaka, alisema Serikali imekuwa ikifanya mikutano na viongozi wa Chama cha
Wafanyakazi wa Reli Tanzania (Trawu) na uongozi wa Tazara na kukubali
kuendelea kutoa huduma huku Serikali ikifanyia kazi matakwa yao.
Dk
Mwinjaka alisema Serikali ya Tanzania imekubali kutoa mshahara wa Aprili
na Februari, huku Serikali ya Zambia ikishughulikia mshahara wa Machi na Mei.
“Tumefikia
hatua kubwa jana (Jumamosi) baada ya mkutano na Chama cha Wafanyakazi na
Menejimenti ya Tazara kuafiki huduma zirejee huku madai yao yakiendelea
kufanyiwa kazi,” alisema.
Aliongeza
kuwa Serikali imeshindwa kusubiri hadi mwisho wa mwezi bila kupatia suluhu
madai ya wafanyakazi hao, kwani haitokua na sura nzuri kwa umma huku wasafiri
wakipata taabu.
“Mshahara
wa mwezi Machi na Mei utashughulikiwa na serikali ya Zambia,” alisema.
Alisema
katika mkutano utakaofanyika mwisho wa mwezi huu, Serikali ya Tanzania itapata
fursa ya kujua ni kwa nini mshahara wa Machi haujawafikia wafanyakazi wa
Tazara.
Mgomo
wa wafanyakazi wa Tazara ulianza wiki iliyopita kwa kudai kulipwa mishahara yao
ya Februari pia Machi, April i2014, ambapo walisisitiza kuendelea kugoma
hadi walipwe.
No comments:
Post a Comment