Kambi
rasmi ya upinzani bungeni imeunda upya baraza lake kivuli la mawaziri kwa
kuingiza wabunge wa vyama vya CUF na NCCR-Mageuzi isipokuwa TLP na DP.
Kiongozi
wa kambi hiyo bungeni, Freeman Mbowe alitaja orodha ya mawaziri vivuli jana mjini Dodoma kwenye mkutano na waandishi
wa habari.
Katika
baraza hilo ambalo Mbowe alisema ni taswira ya Ukawa-bungeni, litakuwa na
mawaziri vivuli 28 na manaibu 12 na kufanya jumla ya mawaziri hao kuwa 40 dhidi
ya 51 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Baraza
hilo linaundwa na wabunge 25 wa Chadema chenye wabunge 49. CUF chenye wabunge
35 kimepata nafasi 11 kwenye baraza hilo na
NCCR-Mageuzi chenye wabunge
watano, wabunge wanne ndiyo wameingizwa
kwenye baraza hilo kivuli.
“Tunaonesha
kwa vitendo azma ya kushirikiana. Tunaonesha kupitia Ukawa ndani ya Bunge,” alisema Mbowe.
Akizungumzia
kutowahusisha Augustine Mrema wa TLP na John Cheyo wa UDP, Mbowe alisema kwa
upande wa Cheyo, upo wakati watahitaji busara zake watamshirikisha. Lakini kwa
upande wa Mrema alisema hana dhamira ya kuwa mshirika wao.
Alipoulizwa
kuhusu kitendo cha Chadema kubeza serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar na
kutaja CUF kuwa imefunga ndoa na CCM, Mbowe alisema, “ni kweli CUF na Chadema
tulitofautiana. Mungu kasaidia Katiba imetuunganisha na sote tuna malengo
sawa.”
Kuhusu
mpango wa vyama hivyo kuendelea na
ushirikiano na hatimaye kusimamisha mgombea mmoja katika uchaguzi mkuu ujao,
Mbowe alisema, “Sisi ni binadamu. Kuna hoja ya kutamani jambo na kuna hoja ya
uhalisia.”
Wizara na wabunge walioteuliwa kuziongoza ni
Ofisi ya Rais yenye mawaziri vivuli watatu ambao wote wanatoka Chadema.
Mawaziri
hao na wizara zao kwenye mabano ni Profesa Kulikoyela Kahigi (Utawala Bora),
Vincent Nyerere (Menejimenti na Utumishi wa Umma) na Esther Matiko aliyepewa
Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu).
Ofisi
ya Makamu wa Rais (Mazingira) itakuwa chini ya Mchungaji Israel Natse (Chadema)
ambaye atasaidiana na Asaa Othman Hamad (CUF).
Ofisi
ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) amepewa Pauline Gekul (Chadema), Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Uratibu na Bunge) itaongozwa na Rajabu Mohamed Mbarouk (CUF) na Tamisemi ni David Silinde (Chadema).
Mbowe
alitaja mawaziri vivuli wengine ni Meshack Opulukwa (Chadema) ataongoza Wizara
ya Kilimo na Ushirika, John Mnyika ataongoza Nishati na Madini akisaidiana na
Raya Ibrahim (Chadema).
Alimtangaza
Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, James Mbatia kuwa Waziri wa Fedha na Uchumi,
akichukua nafasi ya Kabwe Zitto, Mbunge wa Kigoma Kaskazini. Naibu wa Mbatia
atakuwa Christina Lissu.
Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itaongozwa na Ezekiah Wenje
(Chadema) na Haroub Mohamed (CUF). Tundu Lissu (Chadema) ni Waziri Kivuli wa
Katiba, Sheria na Muungano akisaidiana na Rashid Abdallah (CUF).
Felix
Mkosamali (NCCR-Mageuzi) amepangiwa Wizara ya
Ujenzi. Kwa upande wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, amepewa Mbunge wa
Viti Maalumu, Magdalena Sakaya (CUF) na Wizara ya Uchukuzi imekuwa chini ya
Moses Machali (NCCR-Mageuzi).
Wengine
ni Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) anayeongoza Wizara ya Mambo
ya Ndani kwa kusaidiana na Khatib Said Haji (CUF). Halima Mdee (Chadema) anaendelea
kuongoza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Aidha
katika orodha hiyo ya Ukawa, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi inaongozwa
na Rose Kamili (Chadema) pamoja na Mkiwa Kimwanga (CUF).
Maliasili
na Utalii inaongozwa na Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa wakati Ushirikiano
wa Afrika Mashariki inaongozwa na Joseph Selasini (Chadema) pamoja na Rukia
Ahmed Kassim (CUF).
Mbowe
pia alimtaja, Masoud Abdallah Salim (CUF) kuwa waziri kivuli wa Wizara ya
Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Wizara
ya Elimu ameendelea kuwa Suzan Lyimo (Chadema) akisaidiana na Joshua Nassari.
Mbunge wa Biharamulo Gervas Mbassa (Chadema) amekuwa Waziri ya Afya na Ustawi
wa Jamii akisaidiana na Conchesta Rwamlaza (Chadema).
David
Kafulila (NCCR-Mageuzi) amepewa wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko. Habib
Mnyaa (CUF) anaongoza Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia akisaidiana
na Lucy Owenya (Chadema).
Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inaongozwa na Baruan Salum (CUF)
atakayesaidiana na Subreena Sungura (Chadema). Wizara ya Kazi na Ajira
inaongozwa na Cesilia Pareso (Chadema). Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ akiendelea
kuongoza Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
No comments:
Post a Comment