Waziri wa
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara amewataka wananchi kusimama imara kutetea
Katiba mpya na kuwaacha watu
wanaopandikiza mbegu ya kukataa Muungano.
Alisema hayo
jana Dar es Salaam, alipozungumza na wananchi
kwenye maadhimisho ya Siku ya Uanuwai wa Utamaduni Duniani, ambapo maonesho yanayoambatana na siku hiyo,
yalianza kufanyika kuanzia jana hadi Jumapili ijayo.
Alisema Muungano
ni moja ya utamaduni wa Tanzania ambao unatakiwa kuenziwa kama ilivyo kwa
tamaduni nyingine za Watanzania.
Dk Mukangara
alisema Taifa lipo katika mchakato wa kupata Katiba mpya na uanuwai wa utamaduni unakumbusha kuwa mjadala
na mabadilishano ya mawazo vinapaswa kuzingatia usawa na kuheshimiana.
Maadhimisho haya
yamebeba kaulimbiu ya ‘Tudumishe amani, tuuenzi Muungano wetu’, ambapo Dk
Mkangara alitaka kauli mbiu hiyo itumike kulinda na kuhamasisha watu kuenzi
Muungano kwani ni tunu imara katika ulinzi na usalama wa Taifa letu.
Aidha, alitoa
mwito kwa watanzania kuendeleza uanuwai wa utamaduni kwa kushiriki katika
shughuli za maadhimisho hizo.
“Wajasiriamali wa bidhaa za sanaa wanatakiwa kuzalisha
na kuuza bidhaa zao ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuinu akipato chao, vivyo
hivyo kwa wasanii wanatakiwa kukuza vipaji vyao na kuitangaza sanaa ya Mtanzania,’’
alisema Mukangara.
No comments:
Post a Comment