Benki
ya Exim Tanzania imekabidhi maabara ya kompyuta kwa Shule ya Msingi Kilakala
iliyopo wilayani Temeke, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za
kijamii katika kukuza uwezo wa maendeleo miongoni mwa vijana nchini.
Akizungumza
wakati wa makabidhiano hayo jana shuleni hapo, Meneja wa Benki ya Exim Tawi la
Temeke, Joyce Sinamtwa, alisema msaada huo wa maabara ya kompyuta,
unadhihirisha jitihada za benki hiyo katika kuwajengea uwezo vijana wa
Kitanzania kwa kuwekeza katika rasilimaliwatu bora ya baadaye.
"Mbali
na maktaba iliyowekwa mwaka jana, maabara hii ya kompyuta pia itasaidia
kuwaletea maendeleo watoto hawa na kuonesha dhamira yetu ya kuwekeza katika
viongozi wa baadaye wa Taifa hili.
“Baadhi
ya wanafunzi hawa wana uwezo mkubwa wa kufikiri, lakini wanakosa fursa ya
kupata vifaa kama hivi vya kielimu. Benki ya Exim imeamua kuwajengea uwezo
zaidi katika kuwafungulia njia wanafunzi hawa ili kukabiliana na changamoto za
kimaendeleo hapo baadaye.” Alisema Sinamtwa.
Meneja
huyo alisema uongozi wa benki yake unaamini kwamba kwa kuweka maabara hiyo ya
kompyuta katika shule hiyo, wanafunzi wengi wataweza kutumia fursa hiyo
kuendeleza ujuzi wao na hivyo kuwa wabunifu katika maisha yao ya kielimu na ya
kila siku.
Alifafanua
kuwa tangu benki hiyo iichukue shule hiyo na kuwa mlezi wake Agosti 2012, shule
imekuwa ikipiga hatua zaidi kutokana na misaada mbali mbali iliyotolewa na
benki hiyo, ambayo ni pamoja na ukarabati wa miundombinu, kutoa madawati,
vitabu na vifaa vingine vya kitaaluma.
Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi Kilakala, Abdul Kuratasa alisema, "Ni dhana nzuri
ya kuwajengea mazingira mazuri watoto kuwa wataalamu katika sekta ya sayansi na
teknolojia na kuendana na mabadiliko ya dunia. Sasa nao pia wana nafasi ya
kushindana vilivyo na wanafunzi kutoka shule binafsi. Tunawashukuru Benki ya
Exim kwa uwekezaji huu kwa watoto."
No comments:
Post a Comment