Baadhi
ya wafanyabiashara ndogo wametajwa kuchanganya kemikali na vyakula bila
utaratibu hali inayodaiwa kuhatarisha afya za walaji wa vyakula hivyo.
Makamu
wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal alisema hayo hivi karibuni jijini Dar es
Salaam na kusema taasisi ya saratani ya Ocean Road, imekuwa ikipokea wagonjwa
wapya 5,000 wa saratani.
Alisema
tabia na vitendo hivyo vya kuchanganya vyakula na kemikali, si vya kiungwana.
Ameahidi kwamba serikali itaendelea kusimamia na kuhakikisha matumizi
sahihi ya kemikali yanakuwepo.
Alisema
kemikali zisipotumiwa vizuri, zina madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo
kusababisha ongezeko la ugonjwa wa saratani na maradhi mengine.
Alisema
kemikali hutumika kuzalisha mbolea, dawa za kuulia wadudu, kutengeneza dawa za
hospitalini, ujenzi wa nyumba kama saruji, rangi, mbao na mabati na matumizi
mengine mengi.
Aidha
alisema changamoto kubwa katika hilo ni namna bora na salama ya kutumia
kemikali hizo zisilete madhara kwa afya ya watu na kuziepusha kuingia
kwenye mfumo wa ikolojia na kuchafua mazingira.
Hata hivyo alisema madhara ya kemikali yanaweza kuwa
ya muda mrefu au mfupi kulingana na kiwango kitakachoingia mwilini. Kemikali
zinaweza kuharibu mifumo ya fahamu, damu, uzazi na hata mifupa.
No comments:
Post a Comment