BAJETI YA WIZARA YA KAZI NA AJIRA


HOTUBA YA WAZIRI WA KAZI NA AJIRA MHESHIMIWA GAUDENTIA M. KABAKA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015

A. UTANGULIZI
1.    Mheshimiwa Spika; kutokana na taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii iliyochambua bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira (Fungu 65) na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (Fungu 15), naomba kutoa hoja kwamba, Bunge lako tukufu sasa likubali kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji ya Wizara ya Kazi na Ajira pamoja na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa mwaka 2013/2014. Aidha, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kujadili na kupitisha Malengo na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara  pamoja na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.
2.    Mheshimiwa Spika; awali ya yote ninamshukuru mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kushiriki Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, kwa masikitiko makubwa napenda kujiunga na Waheshimiwa Wabunge

wenzangu kutoa pole za dhati kwa familia, ndugu na jamaa za Waheshimiwa Wabunge wenzetu waliofariki katika kipindi hiki ambao ni Marehemu William Augustao Mgimwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga na Said Ramadhani Bwanamdogo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze. Tunamwomba Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, AMINA!
3. Mheshimiwa Spika; nitumie nafasi hii kukipongeza Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ushindi wa kishindo uliopatikana katika uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni wa Wabunge na Madiwani katika maeneo mbalimbali nchini. Ushindi huo ni ushahidi tosha kwamba wananchi wanaendelea kukiamini na kukienzi Chama Cha Mapinduzi. Kwa namna ya pekee niwapongeze Waheshimiwa Wabunge waliochaguliwa katika kipindi hiki; Mheshimiwa Mahamoud Thabit Kombo wa Jimbo la Kiembe-Samaki, Zanzibar; Mheshimiwa Godfrey Mgimwa wa Jimbo la Kalenga, Iringa; na Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete wa Jimbo la Chalinze.
4. Mheshimiwa Spika; naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuendelea kutuongoza na kutoa maelekezo katika kuimarisha viwango vya kazi, uboreshaji wa maslahi ya wafanyakazi, ushirikishwaji wa wafanyakazi na ukuzaji wa ajira nchini. Mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wake yamewezesha kuendelea kuwa na utulivu katika sekta ya kazi hali ambayo imesaidia kukua kwa uchumi wa nchi yetu na kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje kuja kuwekeza nchini kwetu na hivyo kukuza ajira kwa makundi mbali mbali ya wananchi katika nchi yetu na hivyo kuwapunguzia umasikini. Tunaomba Mwenyezi Mungu azidi kumjalia afya njema, maarifa na hekima katika kuiongoza nchi yetu kwa amani na utulivu.
5. Mheshimiwa Spika; napenda pia kwa namna ya pekee kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa imani yake kwangu na heshima kubwa aliyoionesha ya kuendelea kunipa nafasi ya kuiongoza Wizara hii muhimu kwa maendeleo na ustawi wa nchi yetu ya Tanzania.
6. Mheshimiwa Spika; napenda kumshukuru Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Stephen Masatu Wasira, Mbunge wa Jimbo la Bunda kwa hotuba zao nzuri zilizoelezea vema mwelekeo wa Bajeti ya Serikali katika mwaka wa fedha wa 2014/2015. Malengo, maelezo na vigezo vilivyomo kwenye hotuba hizo vimezingatiwa kikamilifu katika kuandaa bajeti ya Wizara yangu kwa mwaka 2014/2015.
7. Mheshimiwa Spika; kwa namna ya pekee ninapenda kutumia fursa hii kuishukuru Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Said Mohamed Mtanda, Mbunge wa Mchinga, Lindi na Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Kapteni John Damiano Komba, Mbunge wa Mbinga Magharibi iliyojadili na kuyakubali Makadirio ya Matumizi ya Wizara yangu. Wizara yangu imezingatia ushauri walioutoa ambao umesaidia sana kuiboresha bajeti hii ninayoiwasilisha leo mbele ya Bunge lako tukufu.
8. Mheshimiwa Spika; Hotuba yangu imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Sehemu ya kwanza ni Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2013/2014. Sehemu ya pili ni Mpango na Bajeti ya Utekelezaji wa Malengo ya Wizara kwa mwaka 2014/2015 na maombi ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango huo.
B. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KAZI KWA  MWAKA 2013/2014
9. Mheshimiwa Spika; Wizara yangu ina jukumu la kuandaa, kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali kuhusu viwango vya kazi, usawa na kazi za staha, ukuzaji wa ajira, ushirikishwaji sehemu za kazi, masuala ya kukuza tija sehemu za kazi na hifadhi ya jamii nchini.

10.Mheshimiwa Spika; katika kutekeleza Mpango Kazi wa Wizara wa mwaka 2013/14 kulingana na majukumu yake, tumezingatia Sera, Sheria, Mipango na Mikakati ya Kitaifa, Maelekezo ya Serikali, Ushauri wa Kamati ya Bunge na Ahadi za Waziri Bungeni wakati akihitimisha Hotuba yake kuhusu Mpango na Bajeti ya mwaka 2013/2014. Katika kipindi hiki tumefanikiwa kutekeleza yafuatayo:­
I. WIZARA YA KAZI NA AJIRA
11. Mheshimiwa Spika; katika mwaka wa fedha 2013/14 Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imetekeleza majukumu yake ya kusimamia viwango vya kazi, ukuzaji wa ajira, ushirikishwaji wa Wafanyakazi sehemu za kazi, kuboresha hifadhi ya jamii na kushughulikia migogoro ya kazi na usalama na afya mahali pa kazi.
12. Mheshimiwa Spika; mwaka wa fedha 2013/ 2014, Wizara (Fungu 65), iliidhinishiwa Bajeti ya jumla ya Shilingi 13,034,148,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo, Shilingi 4,769,301,200 sawa na asilimia 37 zilitengwa kwa ajili ya kulipa mshahara wa Watumishi (PE), na shilingi 8,264,846,800 sawa na asilimia 63 zilitengwa kwa ajili ya matumizi mengine (OC).
13. Mheshimiwa Spika; hadi kufikia tarehe 30 Aprili 2014, Shilingi 4,344,886,775 sawa na asilimia 91 ya fedha za Mishahara ya Watumishi (PE) na shilingi 2,764,106,935 sawa na asilimia 33 ya fedha za Matumizi mengine (OC ) zilitolewa na kutumika na Wizara.

(a) Usimamizi wa Kazi na Huduma za Ukaguzi
Kufanya Ukaguzi Sehemu za Kazi
14. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria za Kazi ambazo ni Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya mwaka 2004 na Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7
ya mwaka 2004. Utekelezaji umefanyika kwa kukagua sehemu za kazi, kutoa elimu ya kuhusu Sheria za Kazi kwa wafanyakazi na waajiri na kuchukua hatua za kisheria kwa wasiozingatia Sheria za Kazi. Aidha, Wizara imeendelea kuwa karibu na Wafanyakazi kupitia vyama vyao na kuhakikisha kuwa inashughulikia matatizo yao kwa wakati. Wizara imeendelea kuhimiza mahusiano mema baina ya Waajiri na Wafanyakazi na kuhamasisha uzuiaji na utatuzi wa migogoro ya kikazi kwa njia ya majadiliano ya pamoja kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kukuza tija mahali pa kazi.
15. Mheshimiwa Spika; katika kipindi hiki, Wizara imekagua jumla ya maeneo ya kazi 1,843 katika sehemu mbalimbali nchini kwa lengo la kuona namna Sheria za kazi zinavyozingatiwa. Katika ukaguzi huu, baadhi ya Waajiri waligundulika kukiuka na kutokutekeleza Sheria zinazohusiana na viwango vya kazi, haki za msingi za kazi pamoja na haki za kuanzisha na kujiunga na vyama vya wafanyakazi katika sehemu za kazi.
16. Mheshimiwa Spika; Waajiri waliobainika kutokuzingatia Sheria na viwango vya kazi walichukuliwa hatua mbalimbali za kisheria. Waajiri 11 walifikishwa mahakamani ambapo waajiri watatu
walitozwa faini ya jumla ya shilingi 2,900,000, waajiri wawili waliamuriwa kulipa haki za wafanyakazi wao jumla ya shilingi 21,000,000 na waajiri 78 walipewa Amri tekelezi (Compliance order).
17. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kutoa elimu kuhusu Sheria za Kazi kwa wafanyakazi na waajiri katika maeneo mbalimbali ya kazi nchini. Elimu hiyo ilitolewa kwa Wafanyakazi 8,201 na Waajiri 412 wa sekta za Viwanda na Biashara, Afya, Kilimo, Ujenzi, Huduma za Hoteli, Ulinzi binafsi, Madini na Usafirishaji.

Kima cha Chini cha Mshahara katika Sekta Binafsi
1.    Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kushughulikia suala la kuboresha maslahi ya wafanyakazi katika sekta binafsi. Kufuatia kutangazwa kwa viwango vya kima cha chini cha mishahara katika Sekta mbalimbali kupitia Tangazo la Serikali No. 196 la tarehe 28/06/2013, Wizara imepokea na kutatua malalamiko 17 kutoka kwa waajiri na wafanyakazi yaliyohusu upangaji na utekelezaji wa viwango hivyo vya kima cha chini cha mshahara.
2.    Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kuhamasisha wafanyakazi na waajiri kujadiliana kwa pamoja katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Katika kipindi hiki jumla ya Mikataba ya Hali Bora 53 ilisainiwa na kusajiliwa na Kamishna wa Kazi ikihusisha sekta za Viwanda, Maji, Biashara pamoja na Hoteli.

Fidia kwa Wafanyakazi (The Workers Compensation Fund)
20. Mheshimiwa Spika; Wizara imekamilisha kanuni za tozo ambapo Waajiri wote wa sekta ya Umma na Binafsi watachangia katika kuendesha Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi. Hii ni kwa mujibu wa Kifungu cha 74(1) cha Sheria ya Mfuko huu Fidia kwa Wafanyakazi ya mwaka 2008 (The Workers Compensation Act, 2008). Mfuko wa utaendeshwa kwa kutumia mfumo wa bima na pensheni kwa kutoa mafao kwa watumishi watakaoumia, kupatwa magonjwa yanayosababishwa na mazingira ya kazi au kufariki mahali pa kazi. Mfuko huu utaanza utekelezaji mwaka 2014/2015.
Hifadhi ya Jamii
21. Mheshimiwa Spika; Katika kuendelea kuimarisha na kupanua huduma za hifadhi ya jamii, Wizara kwa kushirikiana na SSRA imewezesha ziara za mafunzo na kupata uzoefu nje ya nchi kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Watumishi wa Wizara na SSRA katika nchi za Kenya, Uganda, Thailand, Indonesia, China na India. Uzoefu uliopatikana utaiwezesha Wizara na SSRA kuandaa mapendekezo ya kuboresha na kupanua huduma za Hifadhi ya Jamii nchini.
Vita dhidi ya Ajira Mbaya kwa Mtoto
22. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kuratibu juhudi za kukomesha utumikishwaji na ajira mbaya kwa watoto. Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO), chini ya ufadhili wa Serikali ya Brazili, imetoa Mafunzo kuhusu Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza utumikishwaji wa watoto kwa watumishi 35 wa taasisi zisizo za kiserikali na watumishi 190 wa Halmashauri za Wilaya za Simanjiro, Karatu, Lushoto, Kilombero, Mbeya Mjini, Songea Mjini, Dodoma, Singida, Nzega, Tabora Mjini, Kigoma, Kahama, Kishapu na Nyamagana. Aidha, katika kipindi cha sasa hadi Juni, 2014 mafunzo haya yataendelea kutolewa kwa watendaji wa Halmashauri za Wilaya za Iringa, Mufindi, Makete, Iramba, Chamwino, Arusha, Hai, Chunya, Sumbawanga, Musoma, Bariadi, Rufiji, Pangani, Sengerema, Mvomero na Mpanda.
23. Mheshimiwa Spika; Wizara kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali ya “Plan International” na “WEKEZA” yanayotekeleza miradi ya kukomesha utumikishwaji wa watoto katika mikoa ya Geita, Kigoma na Tanga imeweza kuwazuia watoto 3,016 wakiwemo wavulana 1,611 na wasichana 1495 wenye umri kati ya miaka 5 – 13 kuingia kwenye utumikishwaji. Aidha, jumla ya watoto 2,232 wakiwemo wavulana 1,137 na wasichana 1,095 walitolewa kwenye utumikishwaji. Watoto hawa walipatiwa misaada ya vifaa vya shule na kuwawezesha kuingia shule za msingi na shule za ufundi.

Ushirikishwaji wa Wafanyakazi
24. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi kuhusu ushirikishwaji wa wafanyakazi sehemu za kazi. Hatua hii imesaidia sana kuboresha mahusiano na kuwepo hali ya utulivu katika maeneo ya kazi. Aidha, kutokana
na elimu iliyotolewa Wizara ilitatua jumla ya migogoro 9 iliyopokelewa kutoka kwa waajiri wa sekta za Viwanda, Ujenzi na Usafirishaji walio katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Mwanza, Musoma na Kigoma.
25. Mheshimiwa Spika; katika kuimarisha ushirikishaji wa wafanyakazi nchini, Wizara iliratibu kikao kimoja cha viongozi wa vyama vya Wafanyakazi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali kuhusiana na hali na maslahi ya wafanyakazi nchini.
(b) Ukuzaji wa Ajira Nchini
26. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea na juhudi za kuratibu sekta mbalimbali katika kukuza ajira nchini kulingana na Sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2008 na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo nchini. Hadi kufikia mwezi Aprili 2014 jumla ya ajira 630,616 zilizalishwa. Ajira hizo zilizalishwa katika sekta zifuatazo: Kilimo ajira 130,974; Elimu ajira 36,073; Ujenzi wa Miundombinu ajira 32,132; Nishati na Madini ajira 453; Afya ajira 11,221. TASAF ajira 8,686; na Sekta nyingine Serikalini ajira 2,321; Sekta binafsi ajira 211,970; Viwanda vidogo
na vya kati (SMEs) ajira 7,192; miradi ya uwekezaji kupitia Maeneo Huru ya Uwekelezaji (EPZ) ajira 26,381; mawasiliano ajira 13,619; na miradi kupitia kituo cha uwekezaji (TIC) ajira 149,594.
27. Mheshimiwa Spika; Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) katika juhudi za kuwajengea vijana uwezo wa kuwawezesha kujiajiri wenyewe katika maeneo yao, imetoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana 11,500 kupitia Mradi wa Kazi Nje Nje katika Mikoa 17 ya Tanzania Bara. Mafunzo hayo yalilenga katika kubadili fikra za vijina kuwa ajira ni pamoja na kujiajiri, kuwajengea uwezo vijana katika kutambua fursa zilizopo, namna bora ya kuandaa miradi, kutafuta masoko na kutunza mahesabu ya biashara.

28.Mheshimiwa Spika; Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO), pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Kuondoa Umasikini Nchini (REPOA), iliandaa kongamano la kitaifa la kukuza ajira kwa vijana mwezi Desemba, 2013. Kongamano hilo lililozinduliwa na kuongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Gharib Bilal lilihusisha vijana na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na; Waheshiwa Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Vikundi vya Vijana; Wanataaluma, Wataalamu mbalimbali na Washirika wa Maendeleo. Kongamano lilijadili changamoto, fursa zilizopo na kubadilishana uzoefu katika kukuza ajira kwa vijana nchini. Mapendekezo yaliyotolewa katika Kongamano hilo yalitumika kuboresha Mpango wa utekelezaji Programu ya Kukuza Ajira kwa Vijana.
29.Mheshimiwa Spika, Wizara imeratibu ushiriki wa wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi 193 katika Maonesho ya 14 ya Nguvu Kazi/Jua Kali ya Afrika Mashariki yaliyofanyika mjini Nairobi, Kenya mwezi Desemba, 2013. Lengo la ushiriki huo lilikuwa ni kuwapatia fursa wajasiriamali hao kujifunza mbinu na teknolojia mpya zinazotumiwa na wajasiriamali wa nchi jirani katika kuboresha bidhaa wanazozalisha pamoja na kupata masoko mapya ya kuuza bidhaa zao ili kukuza biashara na ajira nchini.
Kuimarisha ukusanyaji taarifa na takwimu za ajira
30.Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kuimarisha utaratibu wa ukusanyaji wa taarifa za ajira nchini kwa kuanzisha mfumo wa kielekitroniki wa kupokea na kutoa taarifa za soko la ajira nchini (Labour Market Information System). Mfumo huu unasaidia kuwaunganisha watafuta kazi na waajiri pamoja na kutoa taarifa za wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu nchini. Mfumo huo unasaidia kutoa taarifa kwa mwekezaji mwenye nia ya kuja kuwekeza nchini popote pale alipo duniani kujua ni aina gani ya ujuzi unaopatikana nchini na hivyo kutokuwa na haja na kuajiri wageni, na hivyo kukuza ajira nchini.

1.    Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu imeendelea kufanya utafiti wa hali ya Nguvu Kazi nchini (Integrated Labour Force Survey). Utafiti huu utatuwezesha kupata taarifa sahihi za hali ya ajira nchini ambayo itasaidia katika kupanga Mipango ya baadae ya kukuza ajira na kupunguza umasikini nchini.
2.    Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Wizara iliandaa mwongozo wa kubaini idadi ya ajira zitakazozalishwa na Wizara, Idara za Serikali, Tawala za Mikoa, Halmashauri na Wakala za Serikali wakati wa kutekeleza bajeti zao za mwaka za miradi ya maendeleo. Kulingana na Mwongozo huo taasisi hizo zinawajibika kutoa taarifa za hali ya ajira katika maeneo yao katika kila kipindi cha robo ya mwaka.

(c) Huduma za Ajira
Wakala wa Huduma za Ajira
33. Mheshimiwa Spika, kufuatia malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi walioajiriwa kupitia Wakala wa Huduma za Ajira, Wizara ilifanya uchunguzi na kubaini ukiukwaji mkubwa wa haki za watumishi ikiwa ni pamoja na malipo hafifu ya mshahara, wafanyakazi kunyimwa haki ya kujiunga na hifadhi ya jamii na haki ya likizo. Kutokana na hali hii, mwezi Disemba, 2013 Wizara ilichukua hatua ya kusitisha utaratibu huu wa kukodisha wafanyakazi. Wizara imeandaa Kanuni za kusimamia shughuli za Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira nchini ambazo zitasimamia ipasavyo Huduma za ajira nchini kulingana na Sheria.
Vibali vya Ajira za Wageni
34. Mheshimiwa Spika, katika kusimamia ajira za wageni nchini kwa lengo la kuhakikisha ajira hizo ni kwa manufaa ya nchi na pia kulinda ajira za Watanzania, mwaka 2013/2014, Wizara  ilipokea na kushughulikia jumla ya maombi 7,432 ya vibali vya ajira za wageni vya Daraja B. Kati ya maombi hayo, maombi 6,237 sawa na asilimia 83.9
yalipendekezwa kupewa vibali, maombi 1,175 sawa na asilimia 15.8 yalikataliwa na maombi 20 sawa na asilimia 0.3 yalisitishwa kwa uchunguzi. Aidha, Wizara imefanya ukaguzi katika kampuni 12 na migodi 6 katika mikoa ya Dar es Salaam, Shinyanga, Mara, Geita na Tabora kwa lengo la kuhakiki vibali vya ajira. Kampuni zilizoonekana kukiuka taratibu zilichukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kusitishwa vibali vyao vya ajira.
35. Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha mapendekezo ya mswada wa Sheria ya Ajira ya Wageni ili kuimarisha na kuongeza ufanisi katika kusimamia ajira za wageni nchini. Sheria itakayotungwa itawezesha kuwepo kwa Mamlaka moja ya kutoa vibali vya ajira kwa wageni ili kuondoa mkanganyiko wa kisheria uliopo kwa sasa unaozipa mamlaka zaidi ya moja katika kutoa vibali vya ajira. Matokeo ya utekelezaji wa Sheria hiyo ni pamoja na kuongeza uwajibikaji katika usimamizi wa soko la ajira nchini na kusimamia ipasavyo ajira za wageni nchini ili kuongeza tija katika kujenga uchumi kupitia uwekezaji.
(d) Usajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri
36. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kuhimiza na kufuatilia haki mbalimbali za Wafanyakazi na Waajiri, ikiwemo haki ya kuanzisha, kujiunga na kushiriki katika shughuli mbalimbali halali za Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri.  Katika mwaka 2013/2014 kazi zifuatazo zimetekelezwa:

i) Kusajili Chama kimoja cha wafanyakazi kijulikanacho kama TAZARA Workers’ Union –Tanzania (TAWUTA) pamoja na Shirikisho la vyama vya walimu vya Afrika Mashariki (FEATU);
ii) Kukagua taarifa za hesabu za vyama 14 vya wafanyakazi, Mashirikisho mawili na vyama viwili vya waajiri;
iii) Kukagua vyama sita katika ngazi ya taifa kuhusu ujazaji wa TUF 6 na TUF 15 kulingana na matakwa ya Sheria;
iv) Kufuta Chama kimoja cha waandishi wa habari (TUJ) baada ya kukiuka masharti ya kisheria; na
v) Kutoa elimu juu ya uhuru wa kujumuika na changamoto zake pamoja na umuhimu wa kuheshimu Katiba za vyama vyao kwa wajumbe wa Vyama vya Wafanyakazi wa Baraza Kuu la THTU, Kamati Kuu ya utendaji ya CWT na Kamati Kuu ya utendaji ya TUCTA.
(d). Kujenga Uwezo wa Wizara
vi) Mheshimiwa Spika; katika kipindi cha mwaka 2013/2014 tumetekeleza yafuatayo katika kujenga uwezo wa Wizara:­
i) Kuajiri watumishi wawili kupitia Tume ya Ajira Serikalini ambao ni Afisa Kazi Daraja la II mmoja na Katibu Mahsusi Daraja la III mmoja;
ii) Wizara imewezesha watumishi 21 kupata mafunzo ya muda mfupi nje ya nchi na watumishi watano ndani ya nchi ili kuongeza ujuzi na utaalamu katika utendaji wao wa kazi. Aidha watumishi wawili wapo kwenye mafunzo ya muda mrefu nje ya nchi na mtumishi mmoja yupo ndani ya nchi.
19
iii) Kuthibitisha ajira za watumishi 14 baada ya kutimiza masharti ya ajira katika kipindi cha majaribio;
iv) Kusimamia zoezi la OPRAS kwa watumishi 279 wa Wizara kulingana na muongozo wa Utumishi wa Umma. Aidha, Watumishi 195 walikamilisha mapitio ya malengo ya nusu mwaka (Julai hadi Desemba, 2013);
II. TAASISI ZA UMMA CHINI YA WIZARA
37. Mheshimiwa Spika; Wizara imeendelea kusimamia shughuli za taasisi sita za umma zilizo chini yake. Taasisi hizo ni Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA), Shirika la Tija la Taifa (NIP), Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA). Utekelezaji wa mipango na kazi kwa mwaka 2013/ 2014 kupitia taasisi hizi ni kama ifuatavyo:
(a) Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA)

1.    Mheshimiwa Spika; Wakala umesimamia na kufuatilia uzingatiaji wa masuala ya usalama na Afya Mahali pa Kazi kwa kufanya ukaguzi maeneo ya kawaida ya kazi 3,626 (General Workplace inspection) ambao ni sawa na asilimia 24.1 ya ukaguzi 15,000 zilizopangwa na ukaguzi maalum 12,290 sawa na asilimia 90.6 ya ukaguzi 13,565 zilizopangwa kufanyika. Ukaguzi huo ulifanywa kwenye maeneo ya umeme, boilers, mitungi ya hewa, zana za kunyanyulia vitu vizito na vipimo vya mazingira. Aidha, wafanyakazi 37,972 walipimwa afya zao sawa na asilimia 101.2 ya lengo la kuwapima wafanyakazi 37,500.
2.    Mheshimiwa Spika; taratibu za kupendekeza kuridhia mikataba mitatu ya Shirika la Kazi Duniani (ILO) kuhusu Usalama na Afya Mahali pa Kazi umefanyika. Mikataba hiyo ni Mkataba Na.155 (Occupational Safety and Health Convention, 1981), Mkataba Na.187 (Promotional Framework for Occupational Safety and Health Convention, 2006) Mkataba Na.167 (Occupational Safety in Construction Convention, 1988).
3.    Mheshimiwa Spika; jumla ya sehemu za kazi 1,671 sawa na asilimia 131 kati ya sehemu za kazi 1,275 zilizopangwa zilisajiliwa. Sehemu za kazi 133 zilipewa vyeti vya kukidhi vigezo vya Sheria Namba 5 ya mwaka 2003 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi.
4.    Mheshimiwa Spika; mafunzo na kozi mbalimbali kuhusu Usalama na Afya Mahali pa Kazi yamefanyika kwa maafisa 1,421 wa afya na usalama mahali pa kazi kutoka sekta mbalimbali. Kozi hizi zinajumuisha kozi ya Taifa ya Usalama na Afya, Kozi ya utoaji wa huduma ya kwanza katika maeneo ya kazi (industrial first aid), usalama katika kufanya kazi za juu (safety in working at height), na kozi ya namna ya kuunda na kuendesha Kamati za Afya na Usalama Mahali pa Kazi.

(b) Wakala wa Huduma za Ajira (TaESA)
42. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 Wizara kupitia Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA) imetekeleza kazi zifuatazo:
i) Kusajili watafutakazi 1,533 na kutembelea waajiri 296. Aidha,
(TIA) na Taasisi ya Teknolojia (DIT) ambapo wahitimu watarajiwa 846 walipata mafunzo ya jinsi ya kukabiliana na Soko la Ajira nchini;
vi) Kutoa ushauri kwa watafutakazi 1,513 juu ya uchaguzi wa fani zinazohitajika kwenye Soko la Ajira na mafunzo ya kazi wanayostahili ili kuwajengea uwezo wa kujiajiri au kuajirika; na
vii) Kujenga uwezo wa watumishi 8 wa taasisi kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika fani mbalimbali.
(c). Shirika la Tija la Taifa (NIP)
1.    Mheshimiwa Spika; katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2013/2014, Shirika la Tija la Taifa (NIP) liliendelea kutoa mafunzo mbalimbali, kufanya tafiti pamoja na kutoa huduma ya ushauri ili kuinua tija sehemu za kazi nchini.
2.    Mheshimiwa Spika; katika mwaka wa fedha 2013/2014, Shirika liliendesha mafunzo 63 ya tija na kujenga uwezo sawa na asilimia 95 ya lengo lililopangwa. Mafunzo hayo yalitolewa kwa

washiriki 630 sawa na asilimia 63 ya lengo. Aidha, tafiti tatu zilifanyika sawa na asilimia 100 ya lengo na kutoa huduma za ushauri katika kukuza tija kwa wateja 8 kutoka Taasisi za umma na binafsi sawa na asilimia 32 ya lengo.
(d). Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA)
45. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2013/14, Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) imetekeleza kazi zifuatazo:
i) Imeshughulikia jumla ya malalamiko 492 yaliyopokelewa kutoka kwa Wanachama na wadau mbalimbali wa sekta ya Hifadhi ya Jamii;
ii) Imeifanyia ukaguzi Mifuko 16 ya Hifadhi ya Jamii kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa Sheria zilizounda Mifuko hiyo na pia Sheria ya Mamlaka, Kanuni na Miongozo yake kama inafuatwa ipasavyo. Kati ya kaguzi hizo, kaguzi nne (4) zilifanyika eneo la kazi (onsite inspection) 12 zilifanyika kwa njia ya taarifa (offsite inspection);
iii) Imetoa elimu kwa watu 7,200 kuhusu Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa makundi mbalimbali ambayo ni pamoja na Wabunge, Watumishi wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, Watendaji wa Vyama vya Wafanyakazi, Vyama vya Waajiri, Vyama visivyo vya Kiserikali (NGOs) na Makampuni binafsi. Aidha, elimu ya Hifadhi ya Jamii ilitolewa kupitia vyombo vya habari kama magazeti (makala 96), runinga (vipindi 24), redio (vipindi 12), mikutano na waandishi wa habari mikutano minne na ushiriki katika maonesho manne (4).
iv) Imetoa Miongozo minne inayohusu taratibu za Mikutano ya Kila Mwaka ya Wanachama wa Mifuko (Conduct of Affairs of the Annual Members Conference Guidelines), Utayarishaji wa taarifa za Mwaka za Mifuko (Annual Reporting Guidelines), Utangamano wa Mifumo ya Mawasiliano ya Mifuko (Interoperability Guidelines) na Ujumuishaji wa vipindi vya kuchangia (Totalization of Periods of Contributions Guidelines) na hivyo kutatua kero za wastaafu 11,000 waliokosa mafao;
hifadhi ya jamii (Extension of Social Security Coverage Strategy).;
xi) Imeanzisha Mfumo wa Kielektroniki wa Mawasiliano kati ya Mamlaka, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, NIDA, na wadau wengine (Core Business Application); kwa lengo la kuboresha mawasiliano katika sekta ya Hifadhi ya Jamii.
xii) Imeandaa rasimu ya Sera ya UKIMWI ya Mamlaka (Institutional HIV/AIDS Strategy);
xiii) Imefanikisha wafanyakazi 24 wa Mamlaka kupata elimu na semina juu ya Ukimwi (HIV AIDS) na masuala ya rushwa (Anti­corruption); na
xiv)Imeanzisha na kuzindua Baraza la Wafanyakazi la Mamlaka.
(e) Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
46. Mheshimiwa Spika; katika mwaka wa fedha 2013/2014 Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limetekeleza kazi zifuatazo:­
i) Limekusanya mapato ya kiasi cha shilingi milioni 705,692.7 sawa na asilimia 74.5 ya lengo na kutumika fedha hizo katika kulipa mafao ya Wanachama, kuwekeza katika vitega uchumi, kulipa gharama za uendeshaji na kuwekeza katika miradi ya maendeleo;
ii) Limeendesha semina 1,931    kwa waajiri na wanachama nchi nzima ili waweze kuelewa vizuri mfumo mpya wa Hifadhi ya Jamii;
iii) Shirika limeandikisha wanachama wapya 80,124 ambao ni asilimia 63.12 ya lengo lililokusudiwa. Aidha, Shirika limelipa mafao mbalimbali ya jumla ya shilingi milioni 235,559.2 ambazo ni asilimia 157.8 ya lengo kwa wanachama 73,742;
iv) Katika kuboresha Huduma kwa Wateja wake; Shirika limepata Cheti cha Kimataifa cha Utoaji Huduma Bora Kwa Wateja (ISO 90001: 2008 Certificate). Aidha Shirika limekamilisha Mpango wa Biashara Endelevu (Business Continuity Management) na pia limeweza kuunganisha Ofisi zake zote za mikoa na Wilaya katika Mkongo wa Mawasiliano wa
29 Taifa (Fibre Cabe), Shirika liko katika hatua za mwisho za maandalizi ya mpango wake wa kupima Afya za baadhi ya wanachama wake (Preventive Health Checks) na kufanya Mkutano Mkuu wa Nne wa wadau wa NSSF mwezi Mei/Juni 2014;
v) Shirika limeshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii (Corporate Social Responsibility) katika maeneo yafuatayo: waliopatwa na maafa ya mafuriko Kilosa, Vikundi vya walemavu; Albino Muungano Investement Trust, Jumuiya ya Upendo Zanzibar na Temeke Albino Group. Huduma za Afya katika ujenzi wa hospitali au Maabara na hata kununua vifaa vya Huduma za afya; Uendelezaji wa Njombe Hospitali, kuboresha Muhimbili – “Paedetric emergency unit”, Kijiji cha Kibamba, Mkuranga, Manispaa ya Temeke na Benjamin William Mkapa “HIV/AIDS Foundation”. Huduma za Elimu katika ujenzi wa shule na Maabara, ununuzi wa madawati na vifaa vya shule, vikiwemo vitanda na magodoro; Shule ya Msingi Mbaya Liwale, Mnyakongo “Educational Development” Manispaa ya Mji wa Iringa
30 – Ismani, Hassan Maajar trust, Kibada Shule ya Msingi, Shule ya Msingi Mhaji, Sumve Girls, Kijiji cha Ibuti Gairo, Ilala Sekondari, Msanga Sekondari, Wama, Nakayama Sekondari, Mwalimu Nyerere Resource Centre na Wilaya za Kahama na Maswa;
vi) Shirika limeendelea na utaratibu wa kutoa mikopo katika Sekta isiyo rasmi (Informal Sector), kwa wanachama wake katika vikundi vya SACCOS na VICOBA ambapo shilingi bilioni 26.16 zimetolewa kwa wanachama 3,341 katika baadhi ya Wilaya zifuatazo: Temeke, Ilala, Kinondoni, Arumeru Mashariki, Singida Mjini, Kigoma, Masasi na Karagwe. Shirika linatoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge, mtumie fursa hii kuwafahamisha watu wajiunge na NSSF ili wapate mikopo.
vii) Shirika linaendelea na Ujenzi wa Daraja la Kigamboni ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2015;
viii)Shirika limeendelea na miradi ya ujenzi wa ofisi na vitega uchumi katika mikoa ya
31 Morogoro, Shinyanga, Kilimanjaro na Wilaya ya Ilala. Aidha, Shirika limeanza ujenzi wa Hoteli ya kisasa katika mkoa wa Mwanza na kuendelea na ujenzi wa jengo la Mzizima, Kijiji cha Kisasa Kigamboni (Tuangoma na Dungu Farm) na nyumba mchanganyiko na ujenzi wa nyumba za bei nafuu Mtoni Kijichi awamu ya tatu; na
ix) Katika miradi inayofanywa kwa ushirikiano na Wadau wengine (Joint Venture Projects); miradi ya ujenzi wa Hospitali ya “Clinic” ya Apollo jijini Dar es Salaam na ujenzi wa ofisi za RITA (Registration, Insolvency and Trusteeship Agency). Ujenzi wa Kijiji cha Bunge Dodoma (MP’s Village), mtaalamu/mwelekezi anakamilisha kuandaa michoro. Aidha, Shirika linasubiri udhamini kutoka Serikali ili kuanza Miradi ya Jengo la Maadili. Na pia katika ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Serikali Nchi nzima, Kampuni ya Watumishi “Housing Limited” inasubiriwa kukamilisha taratibu, ili Shirika liweze kushiriki.
32
III. TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI (CMA)
1.    Mheshimiwa spika, kama ambavyo nimeshaeleza katika aya zilizotangulia, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (Commission for Mediation and Arbitration) ni taasisi ya Serikali  yenye jukumu la kusuluhisha migogoro ya kikazi, kuamua migogoro ya kikazi na kuratibu shughuli za Kamati ya Huduma Muhimu (Essential Services Committee). Vile vile Tume ina jukumu la kutoa elimu ya ushirikishwaji wa wafanyakazi mahala pa kazi.
2.    Mheshimiwa spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (Fungu 15), iliidhinishiwa jumla ya shilingi 2,274, 978,000/-. Kati ya fedha hizo Shilingi 924,978,000/-ni kwa ajili ya mishahara (PE) na Shilingi 1,350,000,000/-ni kwa ajili ya matumizi mengineyo (Other Charges).
3.    Mheshimiwa spika, hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2014, Tume imetumia jumla ya Shilingi 1,272,559,342/-sawa na asilimia 55.9 ya Shilingi 2,274, 978,000/-zilizoidhinishwa na Bunge kwa matumizi ya kawaida.

Utekelezaji wa Majukumu na Kazi kwa Mwaka 2013/14:
50. Mheshimiwa spika, katika mwaka 2013/14, Tume iliendelea kutekeleza majukumu yake kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Taasisi za Kazi Na.7 ya mwaka 2004. Kazi zilizotekelezwa ni zifuatazo:­
i) Kusajili Migogoro 8,584 ambapo migogoro 3,144 sawa na asilimia 37 ilisikilizwa na kupatiwa ufumbuzi. Migogoro 1,935 sawa na asilimia 23 ilimalizika kwa njia ya usuluhishi na migogoro 1,209 sawa na asilimia 14 ilimalizika kwa njia ya uamuzi. Migogoro 2,296 sawa na asilimia 27 inaendelea kushughulikiwa katika hatua mbalimbali za usuluhishi na uamuzi;
ii) Kuwezesha Kamati ya Huduma Muhimu kuainisha maeneo ambayo ni huduma muhimu na kuyasajili. Maeneo yaliyofanyiwa kazi ni pamoja na TANESCO, Maji, Afya na Hali ya Hewa;
iii) Kushirikiana na Shirika la Kazi la Kimataifa (ILO) kutafsiri kitabu cha mwongozo wa kuzuia na kutatulia migogoro ya kikazi (Dispute Prevention and Resolution Training Guide) kutoka katika lugha ya kingereza kwenda lugha ya kiswahili;
iv) Kuwezesha uundwaji wa mabaraza 51 ya Wafanyakazi katika Taasisi mbalimbali ambazo ni Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji (13), na Taasisi za Umma 38 (Wizara, Idara za Serikali, Wakala na Mashirika).
v) Kutoa mafunzo ya kuzuia na kutatua migogoro sehemu za kazi kwa Taasisi 35 ambazo ni Halmashauri 16 za Wilaya, Miji na ofisi za makatibu Tawala za Mikoa (RAS), Taasisi 18  za Serikali (Wizara, Idara, Wakala na Mashirika) na Sekta binafsi;
vi) Imeajiri watumishi wapya 40 katika kada ya waamuzi, wasuluhishi na makatibu muhtasi; na
vii) Imewezesha watumishi 7 kupata mafunzo katika fani ya uhasibu, utawala na ugavi.
Text Box: 35
C. MPANGO WA KAZI KWA MWAKA WA FEDHA 2014/2015
I. WIZARA YA KAZI NA AJIRA
51. Mheshimiwa Spika; katika mwaka 2014/2015 Wizara ya Kazi na Ajira kwa kushirikiana na Taasisi zilizopo chini yake, itaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kusimamia Sheria na viwango vya kazi, ushirikishwaji wa Wafanyakazi na kusuluhisha migogoro sehemu za kazi; kusimamia usalama na afya mahali pa kazi, kukuza na kutoa huduma za ajira; kuboresha ufanisi na tija kazini na kuboresha sekta ya hifadhi ya jamii. Aidha, Wizara itatekeleza mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) unaolenga kuboresha mazingira ya Biashara nchini. Utekelezaji kwa mwaka 2014/ 2015 ni kama ifuatavyo:­
(a) Usimamizi Kazi na Huduma za Ukaguzi
i) Kufanya ukaguzi sehemu za kazi 3,274 ukiwemo wa kawaida, maalum na ufuatiliaji katika maeneo mbalimbali nchini. Lengo ni kuhakikisha kuwa Sheria za kazi zinatekelezwa ipasavyo ili kupunguza migogoro na hatimaye kuongeza tija na uzalishaji. Ukaguzi huo utafanyika katika sekta mbali mbali, kipaumbele kikiwa katika sekta za madini, ulinzi binafsi, huduma za hoteli na majumbani, biashara, viwanda, uvuvi, afya, shule binafsi, mawasiliano na usafirishaji;
ii) Kutoa elimu kuhusu Sheria za Kazi kwa waajiri 1,200 na wafanyakazi 4,000 katika sekta mbalimbali kwa madhumuni ya kuwajengea uelewa wa namna bora ya kutekeleza viwango vya kazi kwa mujibu wa Sheria;
iii) Kuratibu na kukuza majadiliano ya utatu kupitia Baraza la Ushauri la Kazi, Uchumi, na Jamii (LESCO). Katika kipindi hiki Baraza litafanya vikao vyake kwa mujibu wa Sheria ili kuweza kujadili na kutoa ushauri kwa Wizara na Serikali kwa ujumla kuhusiana na masuala ya utekelezaji wa Sheria za kazi, ukuzaji wa fursa za ajira na ukuzaji wa tija na uzalishaji. Wajumbe wa Baraza
37 watajengewa uwezo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi;
iv) Kuratibu na kuboresha upangaji wa kima cha chini cha mshahara katika sekta binafsi kupitia Bodi za Mishahara za Kisekta. Katika kipindi hiki, Bodi zitakazoundwa zitajengewa uwezo na kuwekewa mfumo mzuri wa kutekeleza majukumu yake;
v) Kuendelea na jitihada za kupambana na ajira mbaya kwa watoto kwa kushirikiana na Wizara zenye dhamana ya watoto, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wabia wa Maendeleo na Mashirika yasiyo ya kiserikali. Katika kipindi hiki, Wizara inatarajia kuzuia watoto 4,000 kuingia kwenye ajira mbaya na kuwaondoa watoto 10,000 wanaotumikishwa kwenye ajira mbaya. Katika kufikia malengo hayo, Wizara itatekeleza yafuatayo:
• Kujenga uwezo wa wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Kisekta ya Kuratibu Masuala ya Kupambana na
38 Utumikishwaji wa Watoto nchini na kuiwezesha Kamati kutekeleza majukumu yake,

                Kufanya ufuatiliaji na uratibu wa miradi ya kupambana na utumikishwaji wa watoto katika wilaya za Geita, Sikonge, Urambo, Kasulu, Lushoto na Pangani,
                Kuendelea Kujenga uwezo na kuhamasisha wadau katika ngazi ya Halmashauri za Wilaya ili kuwawezesha kutekeleza Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza Utumikishwaji wa watoto,

vi) Kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) wenye lengo la Kuboresha Uwekezaji na Mazingira ya Biashara nchini kwa kuhuisha Sheria za kazi, kuimarisha ukaguzi sehemu za kazi, uelimishaji kuhusu Sheria za kazi, kuboresha huduma za rasilimali watu na mazingira ya kufanyia kazi;
39
vii) Kuendelea na hatua za kuboresha Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa kuimarisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na kuboresha mafao ya pensheni kwa wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii;
viii) Kuendelea kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii nchini kwa kuanzisha Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi watakaoumia, kufa au kupata magonjwa yatokanayo na kazi. Kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na kuandaa kanuni na miongozo kwa ajili ya kuendesha Mfuko na kujenga uwezo wa Mfuko kutekeleza majukumu yake; na
ix) Kuimarisha utekelezaji wa Maazimio na Mikataba ya Kikanda na Kimataifa kuhusu viwango na masuala mbalimbali ya kazi na ajira kwa kushiriki kikamilifu katika majadiliano, kuridhia Mikataba na kuhuisha Sheria za nchi.
(b) Ukuzaji wa Ajira Nchini
52. Mheshimiwa Spika; Wizara yangu itaendelea kuratibu juhudi za Serikali za kukuza
ajira nchini. Jumla ya ajira 700,000 zinategemewa kuzalishwa katika mwaka 2014/2015 kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo itakayotekelezwa na Taasisi za Umma, Programu ya kukuza Ajira kwa vijana pamoja na hatua mbalimbali za uwekezaji kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC), Mamlaka ya Maeneo Huru ya Biashara (EPZA) na Sekta Binafsi.
53. Mheshimiwa Spika; Ili kukuza ajira na kazi za staha nchini, katika mwaka 2014/2015, Wizara imepanga kutekeleza shughuli zifuatazo:

i) Kuratibu uingizaji wa masuala ya ukuzaji ajira katika mipango na programu za maendeleo za kisekta kwa kutoa mafunzo katika mikoa 3 pamoja na kufuatilia utekelezaji wa mwongozo wa namna ya kuhuisha ukuzaji ajira nchini;
ii) Kusimamia utekelezaji wa Programu ya Kukuza Ajira kwa Vijana ambayo imelenga kuwajengea vijana uwezo wa stadi mbalimbali za kazi na ujasiriamali; kuwapatia vijana mitaji yenye masharti nafuu na nyenzo za uzalishaji; na kutenga maeneo maalum ya uzalishaji, na maeneo ya kufanya biashara. Awamu ya kwanza ya miaka mitatu ya utekelezaji wa Programu hiyo itaanza mwaka wa fedha 2014/ 2015 ambapo jumla ya Shilingi bilioni 3 zimetengwa.
iii) Kuimarisha mfumo wa ukusanyaji na utoaji wa taarifa za soko la ajira nchini; ikiwa ni pamoja na kuratibu ukusanyaji wa taarifa za ajira zinazozalishwa na Wizara, Idara za Serikali, Tawala  za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama ilivyoelekezwa katika Mwongozo wa Bajeti ya mwaka 2014/15;
iv) Kuendelea kufanya Utafiti wa Hali ya Nguvukazi nchini ambao utatoa picha ya hali ya ajira nchini. Utafiti huu utatoa taarifa kuhusu ajira katika sekta rasmi na isiyo rasmi, hali ya utumikishwaji wa watoto, idadi ya ajira mpya zilizozalishwa kwa kipindi cha mwaka 2006 hadi 2014 na matumizi ya muda ya nguvu kazi inayotumika katika uzalishaji mali na utoaji wa huduma.
v) Kuratibu na kuwezesha ushiriki wa wajasiriamali wadogo wa sekta isiyo rasmi 250 wa Tanzania katika Maonesho ya 15 ya Nguvukazi/Juakali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajiwa kufanyika mjini Kigali, Rwanda. Maonesho haya yamelenga kuwapatia wajasiriamali wadogo fursa za masoko, mbinu za kuboresha bidhaa zao, kukuza biashara na kurasimisha kazi na biashara zao hivyo kuongeza ajira kwa wananchi;
(c) Huduma za Ajira
Mheshimiwa Spika; Wizara katika kutoa huduma
za Ajira ilitekeleza kazi zifuatazo:­i) Kukamilisha na kuwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Ajira ya Wageni inayolenga kuimarisha na kuongeza ufanisi katika utoaji wa vibali vya ajira kwa wageni nchini. Aidha, Wizara itaandaa Mfumo wa Kielektroniki wa kutoa vibali vya ajira za wageni nchini kupitia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) unaolenga kuboresha Uwekezaji na Mazingira ya Biashara nchini.
ii) Kuandaa Kanuni na taratibu kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ya ajira ya wageni; na
iii) Kusimamia Kanuni za utoaji wa huduma za ajira zinazotolewa na Mawakala binafsi wa huduma za ajira kulinga na Sheria za nchi;
(d) Usajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri
54. Mheshimiwa Spika; Wizara itaendelea na jukumu la kusajili na kusimamia vyama vya waajiri na wafanyakazi nchini kama ifuatavyo:
i) Kushughulikia maombi ya usajili wa vyama vya Wafanyakazi na Waajiri.
ii) Kufanyia ukaguzi kumbukumbu za wanachama, kuhakiki matumizi ya fedha za vyama na kufuatilia hesabu za mwaka za vyama ambazo zimekaguliwa.
iii) Kuwaelimisha viongozi wa vyama vya wafanyakazi na waajiri juu ya Sheria za kazi na kanuni zake.
iv) Kushughulikia migogoro inayojitokeza kati ya vyama vya waajiri na wafanyakazi .
v) Kushughulikia kesi za mahakamani zinazotokana na maamuzi ya Msajili na masuala yanayohusu Katiba za vyama vya Wafanyakazi na Waajiri; na
vi) Kusimamia utekelezaji wa Katiba za vyama kwa mujibu wa Sheria ya Mahusiano Kazini Na 6 ya mwaka 2004.
(e) Kujenga Uwezo wa Wizara
55. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015 Wizara imepanga kujenga uwezo wa Wizara kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
i) Kuwajengea uwezo watumishi 45 wa Wizara kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi na wengine kumi kuwezeshwa kupata mafunzo ya muda mrefu katika fani mbalimbali;
ii) Kuimarisha mahusiano kazini kwa kufanya vikao viwili vya Baraza la Wafanyakazi na kushiriki katika matamasha ya michezo;
iii) Kuboresha mazingira ya kazi kwa kununua nyenzo na vitendea kazi pamoja na kushirikisha sekta binafsi katika utoaji wa huduma za ulinzi, usafi na matengenezo ya vifaa vya ofisi;
iv) Kuendelea kutoka mafunzo ya Maadili kulingana na Sheria na Miongozo ya Utumishi wa Umma, Vita dhidi ya rushwa, Utawala bora sehemu ya kazi na mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa UKIMWI kwa watumishi 150 wa Wizara. Aidha, Wizara itaendelea kuwahudumia watumishi wanaoishi na virusi vya UKIMWI;
v) Kufanya vikao vinne vya Kamati ya Ajira ya Wizara (mara moja kila Robo Mwaka) kwa kuajiri, kuthibitisha kazini na kupandisha vyeo watumishi 39 wenye sifa za kimuundo na utendaji mzuri wa kazi.
vi) Kuimarisha Ofisi za Kazi za Mikoa ili ziweze kusimamia viwango vya kazi kwa mujibu wa Sheria.
vii) Kuboresha Mifumo ya TEHAMA, Mawasiliano pamoja na tovuti ya Wizara.
TAASISI ZA UMMA CHINI YA WIZARA
56. Mheshimiwa Spika; katika mwaka wa fedha 2014/15 Wizara ya Kazi na Ajira itaendelea kusimamia Taasisi za Umma zilizo chini yake katika kutekeleza majukumu yao kama ifuatavyo:­
(a) Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA)
i) Kufanya ukaguzi sehemu za kazi 20,000 za kawaida na 16,000 maalum kuhusu Afya na Usalama Mahali pa Kazi na kupima afya za wafanyakazi 60,000 katika sehemu mbalimbali za kazi;
ii) Kusajili sehemu 2,000 mpya za kazi ili ziweze kukidhi viwango na kanuni za Afya na Usalama Mahali pa Kazi pamoja na kutoa leseni ya kukidhi matakwa ya Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (The Occupational Health and Safety Act, 2003);
iii) Kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali yanayohusu Afya na Usalama Mahali pa Kazi ambapo mafunzo hayo yatajumuisha kozi ya Taifa ya usalama na afya (NOSHC), kozi ya utoaji wa huduma ya kwanza makazini (industrial first aid), kozi ya usalama katika kufanya kazi za juu (safety in working at height), na kozi ya namna ya kuunda na kuendesha Kamati za Afya na Usalama Mahali pa kazi. Wafanyakazi zaidi ya 1,000 wanatarajiwa kupata mafunzo haya;
iv) Kuanzisha mifumo mbalimbali ya kuboresha utendaji kazi, mfumo wa kutoa taarifa za magonjwa na ajali zitokanazo na kazi, mfumo wa kutunza kumbukumbu, mfumo wa usimamizi wa fedha na mfumo wa usimamizi wa vifaa (Asset tracking system).
v) Kuendelea kuelimisha wafanyabiashara wadogo na wa kati ili waweze kuboresha mazingira ya kazi kwa kuendesha warsha, semina na makongamano mbalimbali katika mikoa ya Tanzania Bara;
vi) Kukamilisha uandaaji wa rasimu za kanuni tatu ambapo kanuni mbili ni
48
kuhusu gesi (“Gas safety installations and use rules”), na (“Vessel under pressure regulations) na kanuni moja kuhusu utoaji taarifa za magonjwa na ajali zitokanazo na kazi (“Recording and reporting of occupational diseases, injuries and dangerous occurrences rules);
vii) Kuendelea kufuatilia hatua za Serikali na Bunge za kuridhia mikataba 6 ya Kimataifa (ILO Conventions) inayohusiana na Usalama na afya mahali pa kazi. Kwa kufuatilia mapendekezo ya kuridhia Mkataba Na. I55 (Occupational Safety and Health Convention, 1981), Mkataba Na.187, (Promotional Framework for Occupational Safety and Health Convention, 2006) Mkataba Na.167 (Occupational Safety in Construction Convention, 1988), Mkataba Na.161 (Occupational Health Services Convention, 1985), Mkataba Na.176 (Safety and Health in Mines Convention, 1995) and Mkataba Na.184 (Safety and Health in Agriculture Convention, 2001).
49
(b) Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA)
57. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015 Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA) umepanga kufanya yafuatayo:
i) Kusajili watafutakazi 2,000 na kuunganisha watafutakazi 1,000 kwa waajiri wenye fursa za ajira ndani ya nchi.
ii) Kutembelea waajiri 1,000 kwa lengo la kubaini idadi na aina ya fursa za ajira.
iii) Kusimamia na kuratibu ajira za Watanzania 1,000 nje ya nchi.
iv) Kuendelea kukusanya, kuchambua na kusambaza Taarifa za Soko la Ajira wa watafuta kazi na waajiri.
v) Kuandaa vipindi 12 vya redio na runinga kwa lengo la kutoa elimu kwa watafutakazi na umma kwa ujumla.
vi) Kuandaa makongamano mawili ya ajira kwa lengo la kukutanisha waajiri na watafutakazi.
vii) Kutembelea taasisi za elimu ya juu 20 kwa lengo la kutoa mafunzo ya jinsi ya kukabiliana na soko la ajira kwa wahitimu watarajiwa.
viii) Kuendeleza rasilimali watu wa Taasisi (TaESA) ili kuongeza tija na ufanisi.
ix) Kutoa ushauri wa kitaalam (consultancy services) kwa wadau juu ya masuala ya huduma za ajira nchini.
(c) Shirika la Tija la Taifa (NIP)
58. Mheshimiwa Spika; katika mwaka wa fedha 2014/15 Shirika la Tija la Taifa limepanga kutekeleza yafuatayo:­
i) Kuendesha mafunzo 80 ya uongozi yatakayohudhuriwa na watumishi 1,200 kutoka taasisi za umma, binafsi na taasisi zisizokuwa za Kiserikali (NGO’s);
ii) Shirika litatoa huduma za ushauri elekezi kwa wateja 30 katika Sekta za Umma, binafsi na zisizokuwa za Kiserikali (NGO’s); na
iii) Shirika litafanya tafiti nne katika maeneo mbalimbali yanayolenga kuboresha tija viwandani.
(d) Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA)
59. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/15 Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii (SSRA) itaendelea na hatua za kuboresha sekta ya Hifadhi ya jamii kwa kutekeleza kazi zifuatazo:
i) Kushirikiana na Wizara ya Kazi na Ajira pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuandaa mapendekezo ya kuanzisha pensheni ya Wazee;
ii) Kuendelea kutekeleza Mkakati wa elimu kwa umma kwa lengo la uongeza uelewa wa masuala ya hifadhi ya jamii. Elimu hiyo itafanyika zaidi kikanda, ambapo zaidi ya wanachama na 15,000 wataelimishwa, vyuo 55 vya maendeleo ya jamii vitafikiwa, na wanafunzi 100,000 wa vyuo vikuu wataelimishwa. Aidha, Mamlaka itaendelea kutumia runinga, redio na magazeti kuwafikia wanachi wengi zaidi nchi nzima;
iii) Kuendelea na zoezi la ukaguzi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili kuhakikisha kuwa Mifuko hiyo inaendesha shughuli zake kwa mujibu wa Sheria na kwa manufaa ya wanachama wake ambao ndio msingi wa kuanzishwa kwa mifuko hiyo. Ukaguzi utafanyika katika maeneo 30 ya kazi, maeneo 6 yakiwa ni Eneo la Kazi (onsite supervision) na maeneo 24 yakiwa si Eneo la Kazi (offsite surveillance);
iv) Kufanya tafiti tatu (3) zenye lengo la kuboresha Sekta ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini.
v) Kuendelea kukamilisha hatua mbalimbali za kuwianisha mafao ya hifadhi ya jamii (benefits harmonization);
vi) Kuendelea na kazi ya usajili wa Mifuko ya hiyari (Supplementary Schemes), Mameneja Wawekezaji (Fund Managers) na Watunza Mali (Custodians) na kutoa miongozo na kanuni za utendaji wao wa kila siku;
vii) Kuandaa mikakati ya kuhamasisha Mifuko iendelee kufanya maboresho ya huduma (products and service re-designing) zote zinazotolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini;
viii)Kuendelea na uandaaji na uhuishaji wa kanuni na miongozo mbalimbali kama ya uhamishaji mafao (transfer of benefits), utendaji wa kila siku wa watoa huduma (Service Providers) zikiwa ni juhudi za Serikali kuhakikisha utoaji mafao bora na kwa wakati;
ix) Kuandaa Mfumo dhabiti wa kusimamia na kukagua Mifuko na watoa huduma (Risk Based Supervisory Framework);
x) Kuandaa na kuratibu maoni ya wadau kuhusu mapendekezo mbalimbali ya mabadiliko ya Sheria ya Mamlaka na Sheria za Mifuko ili kuongeza ufanisi kwenye Sekta;
xi) Kuandaa na kupitia upya kanuni na miongozo mbalimbali ili kuwajengea mazingira bora watumishi na uwajibikaji; na
xii) Kukamilisha uwekaji wa mfumo wa mawasiliano wa kielektroniki baina ya Mamlaka na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (Core Business Application) na kufundisha Mifuko kurekebisha na kutunza takwimu za Wanachama.
(I) Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
60. Mheshimiwa Spika; katika mwaka 2014/15 Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii litatekeleza kazi zifuatazo:­
i) Kukusanya jumla ya Shilingi milioni 1,437,629.1 na kutumia kiasi hicho cha fedha kulipia mafao ya wanachama, kuwekeza kwenye vitega uchumi mbalimbali, kulipa gharama za uendeshaji na kuwekeza katika miradi ya maendeleo;
ii) Kuimarisha uandikishaji na ukusanyaji michango ya Wanachama katika sekta iliyo rasmi na isiyo rasmi (“informal sector”), kuendelea na ukusanyaji wa madeni kwa waajiri na pango kwa wapangaji wa majengo ya NSSF;
iii) Kuendelea kutoa elimu kwa wanachama, waajiri na umma kwa ujumla ili waweze kuelewa vizuri mfumo mpya wa hifadhi ya jamii chini ya NSSF;
iv) Litaendelea na utoaji wa mikopo kwa SACCOS na VIKOBA kwa wanachama wa NSSF;
v) Shirika litaendelea na mpango wa kupima afya za wanachama wake (Preventive Health checks);
vi) Kufanya mkutano mkuu wa tano wa wadau wa NSSF;
vii) Kukamilisha tathimini ya uwezo wa mfuko kifedha ili kulipa mafao kwa wanachama wake kwa muda mrefu ujao;
viii)Kuendelea na mradi wa uzalishaji umeme wa megawati 300 katika eneo la Mkuranga;
ix) Kuendelea na ujenzi wa Daraja la Kigamboni;
x) Kukamilisha ujenzi wa vitega uchumi katika mikoa ya Shinyanga, Morogoro, Kilimanjaro, NSSF/RITA na Wilaya ya Ilala na mradi wa nyumba za bei nafuu 400 Mtoni Kijichi awamu ya Tatu. Pia kuendelea na ujenzi wa Kijiji cha Kisasa Kigamboni (Tuangoma na Dungu “Farm”-“Satellite cities”) na ujenzi wa jengo la Mzizima Towers jijini Dar es Salaam;
xi) Kuanza ujenzi wa jengo kwa ajili ya ofisi ya Makao Makuu katika Mkoa wa Dar Es Salaam, ofisi katika Wilaya za Kinondoni, Temeke, Tarime na Kasulu,  na kuendelea na ujenzi wa majengo ya ofisi na vitega uchumi katika mikoa ya Mbeya, Mwanza, wilaya za Temeke na Kinondoni. Aidha, kuanza kukarabati majengo ya kutunzia kumbukumbu katika Mkoa wa Dar es Salaam; na
xii) Kushiriki katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Appolo, ujenzi wa Vijiji vya kisasa Kigamboni (“Azimio Satellite town” na Geza Satelite Town), ujenzi wa Kijiji cha Bunge Dodoma (MP’s Village) , Ofisi za Bunge Dar es Salaam, Tanga “Commercial Complex”, kituo cha usafirishaji Kigoma, Ujenzi wa Majengo ya NSSF/Maadili, NSSF/TBC na NSSF/NIP.
III. TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI (CMA)
61. Mheshimiwa spika, naomba sasa nitoe maelezo kuhusu mpango wa kazi za Tume ya Usuluhishi na Uamuzi. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/15, Tume imeweka kipaumbele katika kutekeleza yafuatayo:­
i) Kusuluhisha na kuamua migogoro 6,500 ya kikazi na kuandaa taarifa;
ii) Kufanya tafiti juu ya migogoro ambayo haijasajiwa katika Tume na kuishughulikia;
iii) Kuendesha mafunzo 200 ya uelewa na ushauri wa kisheria kwa waajiri na wafanyakazi juu ya kuzuia na kutatua migogoro sehemu za kazi;
iv) Kuandaa na kusimamia vikao vya Makamishna wa Tume na vikao vya kamati ya huduma muhimu (Essential Services Committee);
v) Kuandaa na kusambaza juzuu ya tatu ya kitabu cha rejea cha maamuzi mbalimbali ya Tume (Case Management Guide Vol 3.) yaliyorejewa na Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kwa matumizi ya wadau wa Tume;
vi) Kuwezesha uanzishwaji wa vyombo vya ushirikishwaji wa wafanyakazi mahala pa kazi;
 vii) Kupokea na kusajili mikataba ya kuunda mabaraza ya wafanyakazi sehemu za kazi;
viii) Kufanya tathmini ya hali ya ushirikishwaji Tanzania Bara;
ix) Kujenga uwezo wa Tume kwa kuwaendeleza watumishi kitaaluma; na
x) Kuendeleza mafunzo ya maadili, vita dhidi ya rushwa na utawala bora sehemu za kazi na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI.
D. SHUKRANI
62. Mheshimiwa spika, mafanikio yaliyopatikana katika mwaka wa fedha 2013/2014 yametokana na ushirikiano wa hali ya juu wa viongozi na wafanyakazi wote wa Wizara yangu. Napenda nitumie nafasi hii kuwashukuru Viongozi wote wa Wizara ya Kazi na Ajira pamoja na Mashirika na Taasisi zake, kwa juhudi zao kubwa walizoonyesha katika kutekeleza majukumu tuliyopewa na Taifa.
Shukrani zangu za kipekee nazielekeza kwa
Mheshimiwa Dkt. Milton Makongoro Mahanga (Mb), Naibu Waziri wa Kazi na Ajira na Mbunge wa Jimbo la Segerea kwa ushirikiano na ushauri wake wa karibu. Aidha, napenda pia nitoe shukrani zangu za dhati kwa Katibu Mkuu wa Wizara yangu Bwana Eric F. Shitindi pia ninawashukuru sana Wakuu wa Idara, Vitengo na Watumishi wote wa Wizara yangu, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi zilizopo chini ya Wizara pamoja na Bodi zao kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa majukumu yangu pamoja na michango yao iliyowezesha kuandaa hotuba hii.

63. Mheshimiwa Spika; kwa njia ya pekee naomba niwashukuru Wajumbe wa Baraza la Kazi, Uchumi na Jamii (LESCO), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), kwa michango na ushauri wao mzuri walionipatia katika kutekeleza majukumu na malengo ya Wizara yangu. Nazishukuru pia Wizara na Taasisi, Mashirika na Idara mbalimbali za Serikali na Taasisi zisizo za Kiserikali ambazo tumeshirikiana nazo na sekta binafsi.
64. Mheshimiwa Spika; Wizara yangu inatambua na itaendelea kuthamini michango mbalimbali ya Washirika wa Maendeleo ambayo inasaidia kwa kiwango kikubwa kutekeleza majukumu ya Wizara. Naomba nitumie fursa hii kuzishukuru kwa dhati nchi na Washirika wa
Maendeleo ambao wamechangia katika utekelezaji na mafanikio ya Wizara yetu. Shukrani za dhati ziende kwa Shirika la Kazi Duniani (ILO), UNDP, UNICEF, UNFPA, Shirika la Misaada la Kimataifa la Denmark (DANIDA), Idara ya Kazi ya Marekani, Serikali ya Brazil na Benki ya Dunia.
65. Mheshimiwa Spika; nakushukuru wewe binafsi, Naibu Spika, na Wenyeviti wa Bunge letu kwa kuendesha shughuli za Bunge kwa viwango stahiki. Natoa pia shukurani zangu za dhati kwa Waheshimiwa Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa michango yao ndani ya Bunge na nje ya Bunge inayolenga kuboresha utendaji kazi katika Wizara yangu.
66. Mheshimiwa Spika; kwa namna ya pekee naomba niishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mheshimiwa Said Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Mchinga na Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Kapteni John Damiano Komba, Mbunge wa Mbinga Magharibi kwa kuendelea kuisimamia vyema Wizara yangu. Wizara itaendelea kutekeleza ushauri na maelekezo ya Kamati kwani yanalenga kuboresha utendaji kazi wa Wizara.
67. Mheshimiwa Spika; naomba pia nichukue fursa hii kuwashukuru sana wananchi wote wa mkoa wangu wa Mara kwa ushirikiano mkubwa wanaonipatia. Aidha, kwa namna ya pekee naishukuru familia yangu kwa mchango mkubwa wanaonipatia.

E. MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015
68. Mheshimiwa Spika; naomba sasa kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu liidhinishe jumla ya Shilingi 18,280,136,000 kwa Wizara (Fungu 65) na jumla ya Shilingi 4,683,837,000 kwa Tume (Fungu 15) kwa mwaka wa fedha 2014/2015 ili kutekeleza majukumu na malengo yaliyoelezwa katika hotuba hii katika mchanganuo ufuatao:­
(a) Fungu 65: Wizara ya Kazi na Ajira
i) Shilingi 2,815,205,000 zitatumika kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wa Wizara;
ii) Shilingi 12,464,931,000 zitatumika kugharamia Matumizi Mengine; na
iii) Shilingi 3,000,000,000 ni fedha za maendeleo za ndani kwa ajili ya kutekeleza Programu ya Kukuza Ajira kwa Vijana.
(b) Fungu 15: Tume ya Usuluhishi na Uamuzi
i) Shilingi 1,833,837,000 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi wa Tume, na
ii) Shilingi 2,850,000,000 zitatumika kugharamia Matumizi Mengine.
69. Mheshimiwa Spika; naomba tena nitoe shukrani zangu kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Wizara kwa anwani:
www.kazi.go.tz
70. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

No comments: