Watu
watano wamekufa papo hapo na wengine 16 kujeruhiwa baada ya kutokea ajali ya
barabarani iliyolihusisha gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace
eneo la Mlima Sekenke, wilayani Iramba kwenye Barabara Kuu ya Singida -Mwanza.
Mganga
wa zamu katika Hospitali ya Wilaya ya Iramba, Dk Antony Mbulu,
alisema kuwa ajali hiyo ilitokea juzi saa 2:30 usiku wakati abiria
hao wakienda kwenye sherehe ya Maulid kijiji jirani cha Shelui.
Dk
Mbulu aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni dereva Athuman Adam (34) na
Ally Wambura (36), wakazi wa Igunga na Amin Salim (45) mkazi wa mjini Singida.
Alisema miili ya watu wawili haijatambuliwa.
Kwa
mujibu wa Dk Mbulu, ajali hiyo ilitokea baada ya dereva wa basi hilo lenye
namba za usajili T547 ASP kushindwa kulimudu kutokana na mwendo kasi.
Alisema
kuwa majeruhi watano kati ya 16 waliolazwa kwenye hospitali hiyo, wamehamishiwa
katika Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa matibabu zaidi huku hali zao zikielezwa
kuwa mbaya.
Baadhi
ya majeruhi ambao hawakutaka kutajwa majina yao gazetini, walisema ajali hiyo
ilitokana na mwendo kasi na kutokuzingatia sheria za usalama barabarani.
Walidai
kuwa ajali ilitokea wakati dereva huyo akipita malori kwa kasi, ndipo akagonga
kingo za barabara na kupasua tairi kabla ya kuingia msituni na kupinduka mara
nne. Basi hilo dogo lilikuwa limebeba abiria 21 likitokea mjini Singida kwenda
Shelui.
No comments:
Post a Comment