MFUKO WA PPF WAWAITA WASTAAFU KUHAKIKI TAARIFA

Mfuko wa Pensheni wa PPF  wamewaomba wastaafu ambao taarifa zao  hazijahakikiwa wafike katika ofisi yoyote ya PPF kuhakiki taarifa zao kabla ya Mei  3, mwaka huu.
Meneja Uhusiano na Masoko wa PPF, Lulu Mengele, alisema jana kuwa  Sh bilioni 18 zimekuwa zinalipwa na mfuko huo kwa wastaafu kwa miezi mitatu.
Aliongeza kuwa mfuko huo unahakiki wastaafu wake ambao walikuwa hawajahakikiwa katika mpango wa uhakiki  uliofanyika Mei hadi Agosti, mwaka 2013.
Hivyo alisema uhakiki wa taarifa za wastaafu unafanyika katika ofisi za makao makuu, ofisi za kanda pamoja na ofisi ndogo za mfuko na nyaraka zinazohitajika katika uhakiki huo ni  kitambulisho cha benki, picha ndogo  ya rangi, barua ya Serikali ya mtaa anapotoka, kitambulisho cha Taifa/kadi ya kupiga kura au  leseni ya udereva.
Alisema madhumuni ya kuhakiki wastaafu hao ni kukusanya taarifa za sasa za wastaafu kama vile namba za simu; hivyo kuwa na taarifa  sahihi kwa wastaafu wote na kupata mrejesho kuhusu huduma katika ulipaji mafao.

No comments: