Mkazi wa Kijiji cha Mnyagala, Migu Samweli (46) na binti yake Nsungulwa (15) wamepoteza maisha baada ya kupigwa na radi.
Walikuwa ni wakazi wa kijiji hicho kilichopo katika Tarafa ya Kabungu wilayani Mpanda katika Mkoa wa Katavi na walipigwa na radi wakati wakirejea nyumbani kutoka kwa jirani yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea Aprili 22, mwaka huu , saa 12 jioni kijijini Mnyagala.
Alisema walikwenda kwa jirani yao kumsalimia na ghafla wingu dogo la mvua lilitanda na kulazimu kuondoka kuwahi kurudi nyumbani wasinyeshewe mvua.
"Wakati wakiwa njiani wakielekea nyumbani kwao walipofika jirani na nyumba yao umbali wa meta 15 ndipo walipopigwa na radi na kufa papo hapo. Mama alijeruhiwa vibaya na radi hiyo kifuani na bintie alijeruhiwa vibaya kichwani," alisema Kamanda Kidavashari.
Walikuwa ni wakazi wa kijiji hicho kilichopo katika Tarafa ya Kabungu wilayani Mpanda katika Mkoa wa Katavi na walipigwa na radi wakati wakirejea nyumbani kutoka kwa jirani yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea Aprili 22, mwaka huu , saa 12 jioni kijijini Mnyagala.
Alisema walikwenda kwa jirani yao kumsalimia na ghafla wingu dogo la mvua lilitanda na kulazimu kuondoka kuwahi kurudi nyumbani wasinyeshewe mvua.
"Wakati wakiwa njiani wakielekea nyumbani kwao walipofika jirani na nyumba yao umbali wa meta 15 ndipo walipopigwa na radi na kufa papo hapo. Mama alijeruhiwa vibaya na radi hiyo kifuani na bintie alijeruhiwa vibaya kichwani," alisema Kamanda Kidavashari.
No comments:
Post a Comment