Watu wanane wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga na marungu, wamevamia kambi ya Kampuni ya Wachina.
Wachina hao ni wale wanaojenga barabara inayounganisha Mji wa Mpanda wilayani Mpanda na Kijiji cha Sitalike wilayani Mlele Mkoa wa Katavi na kumjeruhi vibaya mlinzi wa kampuni hiyo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, alisema tukio hilo lilitokea Aprili 22 mwaka huu, saa 5:35 usiku katika kambi ya kampuni hiyo ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, iliyopo Kijiji cha Magamba wilayani Mlele.
Alisema siku hiyo ya tukio, majambazi hao walifika kambini hapo na kumvamia mlinzi huyo, Joseph Sarangi na kumkatakata kwa mapanga na kumpiga kwa marungu. Sarangi amejeruhiwa vibaya usoni na kichwani.
Kamanda Kidavashari alisema majambazi hao waliiba betri ya gari aina ya Nissan yenye Namba 12, kisha kutokomea kusikojulikana.
Alisema Polisi walifanya msako mkali kuhusiana na tukio hilo na walimkamata mtuhumiwa, Juma Athman (23) , mkazi wa Mtaa wa Tambukareli mjini hapa.
Wachina hao ni wale wanaojenga barabara inayounganisha Mji wa Mpanda wilayani Mpanda na Kijiji cha Sitalike wilayani Mlele Mkoa wa Katavi na kumjeruhi vibaya mlinzi wa kampuni hiyo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, alisema tukio hilo lilitokea Aprili 22 mwaka huu, saa 5:35 usiku katika kambi ya kampuni hiyo ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, iliyopo Kijiji cha Magamba wilayani Mlele.
Alisema siku hiyo ya tukio, majambazi hao walifika kambini hapo na kumvamia mlinzi huyo, Joseph Sarangi na kumkatakata kwa mapanga na kumpiga kwa marungu. Sarangi amejeruhiwa vibaya usoni na kichwani.
Kamanda Kidavashari alisema majambazi hao waliiba betri ya gari aina ya Nissan yenye Namba 12, kisha kutokomea kusikojulikana.
Alisema Polisi walifanya msako mkali kuhusiana na tukio hilo na walimkamata mtuhumiwa, Juma Athman (23) , mkazi wa Mtaa wa Tambukareli mjini hapa.
No comments:
Post a Comment