Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya tisa ya siku ya albino, yatakayofanyika Mei 5, mwaka huu.
Maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutafakari vikwazo vinavyosababisha tofauti ya umri wa kuishi kati ya albino na watu wengine.
Ofisa Habari wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner alisema hayo hivi karibuni, jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya "Haki ya Afya, Haki ya Uhai.’’
Alisema maadhimisho hayo ni moja ya mikakati ya kudai haki ya afya kwani kutotekelezwa kwa haki hiyo, ni sawa na kutokidhi haki ya kuishi na kubagua sehemu ya jamii.
Kwa mujibu wa Torner, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe atafungua mkutano wa kimataifa juu ya albino, utakaofanyika jijini Dar es Salaam. Mkutano huo wa siku moja, utafanyika Mei 3 mwaka huu.
Aidha, lengo la mkutano huo ni kupata sauti ya kimataifa kuutaka Umoja wa Mataifa kuitangaza tarehe hiyo kuwa ya kimataifa kwa albino.
Alisema wataalamu kutoka Uturuki, KCMC, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Ocean Road watatoa huduma za upimaji na tiba ya saratani ya ngozi.
Pia, watatoa msaada kisheria kwa watu wote utakaotolewa na Kituo cha Haki za Binadamu na Msaada Kisheria (LHRC).
Maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutafakari vikwazo vinavyosababisha tofauti ya umri wa kuishi kati ya albino na watu wengine.
Ofisa Habari wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner alisema hayo hivi karibuni, jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya "Haki ya Afya, Haki ya Uhai.’’
Alisema maadhimisho hayo ni moja ya mikakati ya kudai haki ya afya kwani kutotekelezwa kwa haki hiyo, ni sawa na kutokidhi haki ya kuishi na kubagua sehemu ya jamii.
Kwa mujibu wa Torner, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe atafungua mkutano wa kimataifa juu ya albino, utakaofanyika jijini Dar es Salaam. Mkutano huo wa siku moja, utafanyika Mei 3 mwaka huu.
Aidha, lengo la mkutano huo ni kupata sauti ya kimataifa kuutaka Umoja wa Mataifa kuitangaza tarehe hiyo kuwa ya kimataifa kwa albino.
Alisema wataalamu kutoka Uturuki, KCMC, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Ocean Road watatoa huduma za upimaji na tiba ya saratani ya ngozi.
Pia, watatoa msaada kisheria kwa watu wote utakaotolewa na Kituo cha Haki za Binadamu na Msaada Kisheria (LHRC).
No comments:
Post a Comment