CHEKA TARATIBU...

Mkulima mmoja kaenda kanisani kwa ajili ya kuomba huduma ya misa kwa ajili ya mbwa wake aliyekufa asubuhi ya siku hiyo. Baada ya kuelezea kwa muda, Mchungaji akamjibu, "Samahani, hatuna huduma hiyo kwa wanyama. Labda kukusaidia nenda mtaa wa pili kuna watu huwa wanafanya maombi wanaweza kukusaidia!" Mkulima kwa furaha akajibu, "Asante sana, nakwenda sasa hivi. Ila unadhani Shilingi Laki Tano inatosha kwa huduma hiyo?" Mchungaji kusikia vile akajibu kwa sauti, "Ebo! Sasa kwanini hukusema mapema kuwa huyo mbwa ni wa dhehebu letu..!?" Duh…

No comments: